1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bayern Munich waanza Bundesliga kwa kuchechemea

19 Agosti 2019

Msimu mpya wa Bundesliga uling'oa nanga wikendi iliyokwisha na usiku wa Ijumaa Bayern Munich walianza kwa kuchechemea kwani licha ya kuwa nyumbani walilazimishwa sare ya magoli mawili na Hertha Berlin.

https://p.dw.com/p/3O8Vi
1. Bundesliga 01. Spieltag | FC Bayern München vs. Hertha BSC Berlin
Picha: Reuters/M. Dalder

Robert Lewandowski ndiye aliyewafungia Bayern magoli yote la pili akilifunga kupitia mkwaju wa penalti kisha Dodi Lukebakio aliyewafunga Bayern msimu uliopita hapo Allianz Arena wakati akiichezea Fortuna Düsseldorf, safari akafunga goli la kwanza la Hertha.

Marko Grujic ndiye aliyefunga bao la pili baada ya mchezo mzuri kutoka kwa Hertha Berlin.

Jumamosi Borussia Dortmund wakawaduwaza Augsburg magoli matano kwa moja uwanjani Signal Iduna Park.

Bundesliga | 1. Spieltag | Borussia Dortmund - FC Augsburg
Dortmund washerehekea bao la Jadon SanchoPicha: Reuters/L. Kuegeler

Paco Alcacer alifunga mabao mawili na wengine walioandikisha majina yao katika daftari la wafungaji ni Jadon Sancho, Marco Reus na Julian Brandt ambaye alifunga katika mechi yake ya kwanza kama mchezaji wa BVB baada ya kujiunga nao katika dirisha la uhamisho lililopita kutoka Bayer Leverkusen.

Augsburg walifungiwa bao la kufutia jasho na Florian Niederlechner.