1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Betancourt

Mtullya, Abdu Said3 Julai 2008

Mwanasiasa wa Columbia Ingrid Betancourt amewasili nyumbani Bogota pamoja na watu wengine waliotekwa nyara na waasi wa Farc.

https://p.dw.com/p/EVCc
Mwanasiasa wa Columbia Ingrid Betancourt mara baada ya kuwasili Bogota.Picha: AP

BOGOTA:

Mwanasiasa  wa  Columbia Ingrid Bentacourt amewasili mji mkuu wa Columbia Bogota, pamoja na mateka wengine 14 waliokombolewa na majeshi ya   Columbia.

Bentacourt  na  mateka  hao  wengine , ikiwa pamoja na wamarekani  watatu walitekwa nyara  na  waasi wa Columbia wanaoitwa  FARC.

Mwanasiasa huyo maaruf  aliewahi kugombea  urais  wa nchi yake alitekwa nyara na waasi hao  miaka zaidi ya sita iliyopita.

Mara baada ya kuwasili  kwenye  uwanja wa ndege  wa kijeshi wa Bogota Bentacourt  ambae pia  ni raia wa Ufaransa  alilakiwa na mama yake na ndugu zake  wengine kadhaa.