1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bin Laden ataka Ulaya iondowe wanajeshi wake Afghanistan

30 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CUwy

Kiongozi wa Al Qaeda Osama bin Laden amezitaka nchi za Ulaya kuondowa wanajeshi wao kutoka Afghanistan.

Kwenye ukanda mpya wa video uliorushwa hewani na kituo cha televisheni cha Kiarabu cha Al Jazeera hapo jana bin Laden amewataka wananchi wa Ulaya kuzishinikiza serikali zao kujitowa Afghanistan.

Bin Laden kwa mara nyengine amekubali kuwajibika na mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11 mwaka 2001 nchini Marekani lakini amesema kundi la Taliban wakati huo likiwa madarakani nchini Afghanistan lilikuwa halijuwi kitu juu ya mipango ya mashambulizi hayo.

Wakati huo huo wanajeshi wawili wa Danmark wameuwawa hapo jana wakati wakipambana na waasi wa Taliban katika jimbo la Helmand kusini mwa Afghanistan.