1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Blinken airai Hamas kuridhia ombi la Israel kuwaachia mateka

29 Aprili 2024

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken amewatolea mwito wanamgambo wa kundi la Hamas kukubali pendekezo la Israel la kuwaachilia huru mateka wanaowashikilia Gaza,ili kufungua njia ya usitishaji mapigano.

https://p.dw.com/p/4fJVc
Marekani | Antony Blinken
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony BlinkenPicha: Ichiro Ohara/Yomiuri Shimbun/AP Photo/picture alliance

Wajumbe wa Hamas wanatarajiwa kukutana na wapatanishi wa Qatar na Misri mjini Cairo,kutoa jibu lao kuhusiana na pendekezo hilo lililowasilishwa mwishoni mwa juma na Israel.

Wakati huohuo Israel imeshambulia katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza na kuua takriban Wapalestina 25 na kuwajeruhi wengine wengi kwa mujibu wa madaktari.