ISLAMABAD: Umwagaji wa damu waendelea Pakistan
19 Julai 2007Matangazo
Si chini ya watu 20 wameuawa nchini Pakistan katika shambulizi la kujitolea maisha muhanga. Shambulizi hilo lililenga msafara wa raia wa Kichina na vikosi vya usalama vya Pakistan. Mripuko huo wa bomu umetokea mji wa Hub katika wilaya ya Baluchistan ambayo tangu takriban miaka mitatu iliyopita imekumbwa na machafuko ya waasi wa kikabila wanaogombea mamlaka ya kujitawala wenyewe.Katika shambulizi jingine la kujitolea maisha muhanga na kulenga taasisi ya polisi,hadi watu 8 waliuawa na 29 wengine walijeruhiwa kaskazini-magharibi ya nchi.