1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KAMPALA:Pingamizi dhidi ya ndoa ya jinsia moja zapamba moto

3 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBTE

Askofu mkuu wa kanisa la Kianglikana nchini Uganda Henry Luke Orombi amemtawaza kasisi wa Kimarekani na kuwa askofu katika wimbi jipya la hatua ya viongozi wa dini ya kikristo wanaopinga ndoa za jinsia moja.

Wimbi hilo pia limekumba kanisa la Kianglikana nchini Marekani na linakabiliwa na kuondokewa na makasisi wanaopinga ndoa hizo za jinsia moja.