1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kansela wa Ujerumani akutana na Waziri Mkuu wa Lebanon

23 Februari 2008
https://p.dw.com/p/DC7o

BERLIN:

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amekutana na Waziri Mkuu wa Lebanon Fouad Siniora mjini Berlin.Merkel ameunga mkono jitahada za upatanisho za Umoja wa Nchi za Kiarabu kuhusika na kuteuliwa kwa rais wa Lebanon ili kuziba pengo la uongozi nchini humo.Kuambatana na mpango mpya wa maafikiano,wadhifa wa urais unatazamiwa kwenda kwa mgombea Michel Suleiman ambae hivi sasa ni mkuu wa majeshi.

Merkel amekariri kuwa Ujerumani itasaidia kujenga upya utaratibu wa kidemokrasia nchini Lebanon.Wakati huo huo akatoa mwito kwa Syria kuchukua hatua zitakazosaidia kutenzua mzozo wa Lebanon.Upande wa upinzani nchini Lebanon unaoongozwa na chama cha Hezbollah cha Washia wenye itikadi kali,unaungwa mkono na Syria.