1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenenisa Bekele ashinda mita 5000 kwa Ethiiopia

23 Agosti 2009

Muafrika kusini Mulaudzi ashnda mita 800 kwa A.kusini.

https://p.dw.com/p/JGuC
Bekele -mta 5000Picha: AP

Mashindano ya 12 ya riadha ulimwenguni katika Uwanja wa olimpk wa Berlin, yanamalziika hivi punde kwa changamoto ya mbio za mita 400X4 wanaume Kenenisa Bekele ashinda mbio za mta 5000 na Rais wa IAAF msenegal Lamine Diack, amesema mashindano ya Berlin yamefanikiwa .

Kenensa Bekele ameshinda hivii punde mbio za mita 5000 wanaume, iingawa alitolewa jasho na Kipchoge wa Kenya na bingwa mtetezi Bernard Lagat wa Marekani aliejipatia medali ya fedha .Kipchoge hakupata medali.

Bekele alimaliza mbo kwa muda wa dakika 13.sek.17.09.Bekele alkwishashinda tajii la mita 10.000.Medal ya shaba iilikwenda kwa James C-Kurui aliekimba kwa niiaba ya Qatar.Baadae ikawa zamu ya mbio za mita 1500 wanawake na kabla ya mita 800 wanaume:

Katika fiinalii ya mta 1500 wanawake, macho yalikodolewa Gelete Burta wa Ethiiopia na akiongoza mbio hizo hadi alipotiwa munda na kuanguka.Natala Rodreguez wa Spainndie aleondoka mshiindi ingawa nii ushindi wa shaka-shaka baada ya kumuangusha Burta wa Ethiopiia. Maryam Yusuf Jamal wa Bahrein alijiipata medali ya fedha.

Afriika Kusini imejpatia medal ya pili ya dhahabu katika mita 800 mara hi upande wanaume.Baada ya ushindi wa Caster Semenya,upande wa wasichana, Mulaudzi amepeleka medali nyengine Afrika kusni. Yusuf Kemel ameipatia Bahrein medali ya pili ya fedha leo baada ya ile ya Maryam Yusuf.Alikwisha shinda medalii ya dhahabu katiika mta 1.500 wanaume. Medalii ya shaba ilienda Kenya.

Leo siku ya mwisho ya mashindano haya ,changamoto ilianza kwa mbio za marathon kwa wanawake.Baada ya kupita saa 2:25 na sek.15, mshindii aliibuka msichana wa China -Xue Bai.Medalii ya fedha, iikaenda kwa mjapani Yoshimi Ozaki aliechukua muda wa masaa 2:25:25.Muethiopia Aselefech, alibidi kusalim amri kwa kasi za wapinzani wake 2 kutoka Asia na kuridhika na medali ya shaba.

Wakati Ethiopia, imefurahia leo medalii ya shaba katika mbio za marathon, jana ilkuwa siku ya wakenya.Walitwaa medali 4-2 za dhahabu na 2 za shaba.Kenya iliitamba katika mbio za mita 5000 wanawake ushindi ukienda kwa Vivan Cheruiyot na medalii ya fedha ikinyakulwa na Sylvie Kibet.

Mashindano ya 12 ya ubingwa wa riadha ulimwenguni, yanahetimishwa hivi punde kwa mbio za kusisimua za mita 400X4.Huo utakuwa msisimko wa mwisho wa mashindano haya baada ya jana Usain Bolt kuwasaidiia wajamaica kutwaa medali nyengine ya dhahabu katika mbio za mita 100X4 kupokezana. Usain bolt alinyakua medali yake ya 3 ya dhahabu. Akiwa shabikii wa dimba wa klabu ya Real Madrid ya Hispania, Real imemualika rasmi mpambano wao wa kwanza msimu huu dhidi ya Depotivo.

Nae Rais wa Shiirikisho la riadha ulimwenguni IAAF,msenegal Lamine Diack,a kizungumza leo siiku ya mwisho ya mashindano, ameyaeleza mashindano ya Berlin kuwa yaliofankiwa mno.Kwani, kama katika michezo ya olimpik ya Beiijing, mwaka jana, Usain bolt ametia tena fora."Tumejionea mashindano ya kusisimua"-alisema Lamine Diack.Kabla changamoto za mwisho leo, nchi 34 ziliingiia katika orodha ya medali-Kenya ikiwa usoni miongonii mwa mataifa ya Afriika. Mashindani yajayo ya ubingwa wa riadha yatafanyika 2011 mjini Daegu,Korea ya Kusni.