1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya: Maandamano ya kupinga nyongeza ya Mishahara kwa wabunge

14 Mei 2013

Nchini Kenya hii leo tarehe 14.05.2013 kunafanyika maandamano ya amani ya kupinga nyongeza ya mishahara ya wabunge.

https://p.dw.com/p/18XK2
Wabunge nchini Kenya wadai nyongeza ya mshahara
Wabunge nchini Kenya wadai nyongeza ya mshaharaPicha: AP

Wabunge nchini humo wanataka tume inayoshughulikia mishahara ya watumishi wa umma iongeze mishahara yao kutoka elfu 532,000 hadi 850,000. Wabunge hao wa Kenya wanasema kima walichoekewa ni kidogo sana kukidhi mahitaji yao.

Hata hivyo tume hiyo imesema haitabadilisha msimamo wake huku ikitupilia mbali vitisho kutoka kwa wabunge hao waliosema wataifuta kazi tume hiyo iwapo matakwa yao hayataridhiwa.

Mwandishi wetu wa Nairobi Reuben Kyama yuko katika maandamano na kwanza anatueleza hali ilivyo kwa sasa.

Mwandishi Amina Abubakar

Mhariri Yusuf Saumu

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi

Gundua zaidi