1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya yang'aa katika riadha Doha

7 Oktoba 2019

Yale mashindano ya dunia ya riadha yaliyokuwa yanaendelea Doha Qatar yalikamilika Jumapili huku Marekani ikiongoza katika nafasi ya kwanza ikiwa na jumla ya medali ishirini na tisa.

https://p.dw.com/p/3QqT4
Leichtathletik-WM Doha 2019 Frauen Finale 5000 Konstanze Klosterhalfen
Picha: REUTERS

Kenya wameiwakilisha Afrika vyema kwa kuinyakua nafasi ya pili wakiwa na jumla ya medali kumi na moja, tano kati ya hizo zikiwa dhahabu.

Rais wa Shirikisho la Riadha Duniani IAAF Sebastian Coe amesema kulikuwa na ufanisi mkubwa.

"Hatujakabiliana na visa vyovyote vibaya, wanariadha walikuja kwenye mashindano haya wakifahamu changamoto zitakazokuwa na kwa sehemu kubwa nafikiri wameshindana vyema sana," alisema Coe.

Uwanja uliotumika kwa mashindano hayo wa Khalifa kwa wakati mwengine ulikuwa hauna mashabiki ingawa makamu wa rais wa kamati andalizi ya mashindano hayo Dahlan Al-Hamad amesema hilo ni jambo la kawaida.

"Kujaza uwanja ni changamoto kwa kila mtu. Tumeiona changamoto hii si katika mashindano haya tu, ni katika karibu mashindano yote. lakini tunafurahia kufika hatua hii," alisema Al-Hamad.