1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kiongozi wa upinzani Sudan aachiliwa

Sekione Kitojo
5 Machi 2019

Kiongozi mwandamizi wa upinzani nchini Sudan aliyekamatwa tangu mwezi Disemba mwaka uliopita kwa kushiriki maandamano ya kumpinga Rais Omar al-Bashir, ameachiliwa huru.

https://p.dw.com/p/3ETYs
Sudan | Protest
Picha: Getty Images/AFP/A. Shalzy

Maafisa  wa  Sudan  wamemuachia  huru  kiongozi mwandamizi wa  upinzani  ambaye alikuwa  amekamatwa tangu  mwezi  Desemba kwa  kuhusika  na  maandamano dhidi  ya  utawala  wa  Rais Omar al-Bashir, chama  chake kimesema  leo. 

Omar el-Digier, mkuu  wa  chama  cha  upinzani  cha Sudanese Congress Party, alikamatwa  na  kufungwa  siku kadhaa  baada  ya  maandamano  kuzuka  Desemba  19 baada  ya  uamuzi  wa  serikali  kupandisha  bei  ya  mkate mara  tatu  zaidi.

Maafisa  walianzisha  ukandamizaji  nchi  nzima  kuzuwia maandamano  wakati  yakiongezeka  nchi  nzima  dhidi  ya Bashir, aliyeingia  madarakani  katika  mapinduzi yaliyoungwa  mkono  na  wanaharakati  wa  Kiislamu mwaka  1989.

Lakini  watu  wengine 40  viongozi wa  vyama  bado  wako gerezani, wakati  ambapo  kiongozi  huyo  aliyeachiwa huru  amesema  kwamba  maandamano  yataendelea dhidi  ya  Rais Bashir.