1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kipchoge: Sikio langu la kulia liliziba

5 Oktoba 2020

Mfalme wa mbio za masafa marefu marathon Eliud Kipchoge kutoka Kenya anasema alishindwa kulitetea taji lake la mbio za London Marathon jana kwa kuwa alipata changamoto mbio zilipokuwa katikati.

https://p.dw.com/p/3jSy8
England | London Marathon | Eliud Kipchoge
Picha: Adam Davy/empics/picture-alliance

"Mbio zilikuwa nzuri nilianza vyema, kulikuwa na baridi lakini nilipata tatizo dogo tu na sikio langu la kulia, liliziba na nilijaribu kulizibua ila haikuwezekana. Ila yote tisa huu ni mchezo na katika michezo leo utakuwa juu kesho utakuwa chini," alisema Kipchoge.

Hii ilikuwa ni marathon ya pili Kipchoge kushindwa katika taaluma yake hiyo ya ukimbiaji wa mbio za masafa marefu.