1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wimbledon yaanza rasmi Jumatatu

1 Julai 2019

Kinyang'anyiro cha Wimbledon katika mchezo wa Tennis kiling'oa nanga Jumatatu huko Uingereza. Macho yote yatakuwa kwa Muingereza Andy Murray aliyerudi kutoka kwenye jeraha lililomuweka nje kwa miezi mitano.

https://p.dw.com/p/3LQ02
Australian Open Tennis - Andy Murray im Spiel gegen Roberto Bautista
Picha: picture-alliance/AP Photo/A. Brownbill

Murray ambaye ni raia wa Scotland ana miaka 32 na anasema hatarajii mengi.

"Ningependa kufanya vyema nitakapokuwa uwanjani. Nacheza kwa ajili ya kupata ushindi na mimi ni mshindani sana. Lakini sijiambii kwamba, wiki nne au tano zilizopita nilikuwa sijui kama ningecheza hapa. Kwa hiyo sitarajii mengi. Lakini mara nitakapoingia uwanjani, nitajaribu kushinda kila mechi nitakayocheza," alisema Murray.

Wakati huo huo Mjapani Naomi Osaka ambaye alikuwa mchezaji nambari moja duniani upande wa kina dada anasema akili yake kwa sasa iko huru kutokana na shinikizo la kuitetea nafasi yake kama mchezaji nambari moja.

Tennis Australian Open Finale Frauen | Naomi Osaka
Osaka kwa sasa anaorodheshwa katika nafasi ya pili dunianiPicha: picture-alliance/AP Photo/M. Schiefelbein

"Ndiyo, kisaikolojia kuwa nambari moja lilikuwa ni shinikizo kubwa sana kuliko nilivyotarajia. Kwa hiyo, ndio, nafikiri ni vyema kwangu kwa sasa kuorodheshwa wa pili hapa kwasababu jambo zuri ni kwamba ukishinda kipute hiki basi moja kwa moja unakuwa nambari moja. Kwa kweli hilo ndilo lengo langu kubwa. Sihitaji kufikiria kuhusu kuitetea nafasi yangu au kitu chochote," alisema Osaka.