1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kobane wakaribia kuangukia mikononi mwa kundi la IS

7 Oktoba 2014

Wapiganaji wa Jihad wako ukingoni mwa kuukamata mji wa mpakani wa Syria wa Kobane, wakati Uturuki ikionya kuwa baada ya mashambulizi ya wiki tatu ya kundi linalojiita Dola la Kiislamu mamia ya watu wameuwawa.

https://p.dw.com/p/1DRhh
Kobane IS Kämpfe Syrien Kurden Flüchtlinge Terrorismus
Bendera ya kundi la IS ikipepea mlimaniPicha: REUTERS/U. Bektas

Kuanguka kwa mji wa Kobane mikononi mwa kundi linalojiita Dola la Kiislamu kutakuwa ni ushindi mkubwa kwa wapiganaji hao wa Jihad, ambao wanapigana ili kumata eneo kubwa la mpaka na Uturuki kwa ajili ya kulitangaza kuwa ni mamlaka ya Ukhalifa.

Kiasi ya watu 412, zaidi ya nusu yao wakiwa ni wapiganaji wa Jihad , wameuwawa ndani na kuzunguka mji wa Kobane tangu katikati ya Septemba, kwa mujibu wa shirika linaloangalia haki za binadamu nchini Syria, shirika lenye makao yake makuu nchini Uingereza.

Kobane IS Kämpfe Syrien Kurden Flüchtlinge Terrorismus
Wapiganaji wa kundi la IS karibu na mji wa KobanePicha: REUTERS/U. Bektas

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameonya kwamba mji huo muhimu kimkakati uko karibu na kuangukia mikononi mwa kundi la IS, akisema operesheni za ardhini za kijeshi zinahitajika kuweza kuwashinda wanamgambo hao.

"Ugaidi hautamalizika ...hadi pale tutakaposhirikiana katika operesheni ya ardhini," Erdogan amesema katika hotuba kwa njia ya televisheni.

Kobane IS Kämpfe Syrien Kurden Flüchtlinge Terrorismus
Wakimbizi wa Kikurdi kutoka mji wa KobanePicha: REUTERS/U. Bektas

Mapigano ya mitaani Kobane

Wakati mapigano kuudhibiti mji wa Kobane yakiingia katika awamu muhimu, wanamgambo wa Kikurdi wakisaidiwa na mashambulizi ya anga ya jeshi la Marekani wamepambana katika mapigano ya mitaani na wanamgambo hao wa Jihad waliokuwa wakisonga mbele, ambao wamevunja ulinzi wa mji huo jana Jumatatu.

Milio ya risasi na miripuko pamoja na ngurumo za ndege za kijeshi vilisikika kutoka upande wa mpaka wa Uturuki, wakati bendera ya Wakurdi ikionekana ikipepea katikati ya mji wa Kobane, kwa mujibu wa mwandishi habari wa shirika la habari la AFP.

Kobane IS Kämpfe Syrien Kurden Flüchtlinge Terrorismus
Moshi mkubwa ukitoka kutoka mji wa KobanePicha: Reuters/Umit Bektas

"Tunahitaji msaada kutoka katika jumuiya ya kimataifa," Idris Nahsen afisa wa Kikurdi ambaye bado yuko mjini Kobane amesema . "Ama tuwamalize IS ama watatumaliza," ameongeza.

Raia watakiwa waondoke Kobane

Wapiganaji wa Kikurdi wamewaamuru raia kuondoka kutoka mji huo, baada ya wapiganaji wa Jihad kuweka bendera zao nyeusi upande wa mashariki na kuingia mjini Kobane jana Jumatatu.

Kundi la IS ni la Wasunni wenye itikadi kali , na limefadika na mparaganyiko uliotokea kutokana na makundi kadhaa nchini Syria kuingia vitani kupambana na utawala wa Syria , na wakakamata maeneo makubwa , pamoja na maeneo ya nchi jirani ya Iraw.

IS Flagge vor Kobane Syrien Türkei Grenze Detail Ausschnitt
Bendera nyeusi ya kundi la ISPicha: Reuters/Umit Bektas

Kaskazini magharibi mwa Syria , wakati huo huo kundi hasimu dhidi ya Dola la Kiislamu lenye itikadi kali lenye mafungamano na al-Qaeda la Al-Nusra Front, limemkamata kasisi mmoja na Wakristo kadhaa usiku wa Jumapili, wamesema wamisionari wa Franciscana leo.

Mwandishi: Sekione Kitojo / afpe /dpae

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman