1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magazetini: Siasa za kizalendo barani Ulaya

Sekione Kitojo
5 Julai 2018

Wahariri wa magazeti ya Ujerumani wamejishughulisha na mada kuhusu mwelekeo wa siasa za kizalendo barani Ulaya,chama cha SPD chalalamikia kuhusu vituo vya kuwahifadhi wakimbizi,na hatua za uokozi wa vijana huko Thailand.

https://p.dw.com/p/30sYl
Protest gegen Ankerzentren - Bayerisches Transitzentrum Manching
Waandamanaji wakipinga vituo vya kuwashikilia wakimbizi vinavyotakiwa na chama cha CSU jimboni BavariaPicha: picture-alliance/dpa/S. Puchner

Mhariri  wa  gazeti  la  Volksstimme  la  mjini  Magdenburg akizungumzia siasa za kizalendo  zinavyoshika  kasi  barani  Ulaya anasema, kwamba  sehemu  kubwa  ya  siasa  za  Ujerumani zinaelekea kuwakashifu  majirani  zetu  wanaojionesha  kuwa wanakumbatia  siasa  za  kizalendo: Mhariri  anaandika:

"Hususan katika  Ulaya mashariki mara  nyingi hutupiwa  lawama. Hii ni  kutokana  na  mageuzi  ya  mfumo  wa  mahakama  nchini  Poland , suala  ambalo  limekuwa  likiishughulisha  kwa  muda  mrefu Halmashauri  ya  Umoja  wa  Ulaya. Hapana  mhariri  anaandika kwamba  Ujerumani  haina haki  ya kushikilia  masuala  ya  kimaadili na uwajibikaji  katika  Umoja  wa  Ulaya. Si  haki kwa, wakati  ukweli uko  wazi  kwamba  hali  inabadilika  kuhusu  uzalendo  nchini Ujerumani  na  unakandamizwa tu. Kutokana  na  chama  cha  AfD na hali isiyoshwari kwa  wananchi  muungano  unaounda  serikali  umo katika  hali ya kutafunana kutokana  na  sera  za  uhamiaji, Ulaya imo  katika  hatari  kubwa."

Mhariri  wa  gazeti  la  Rheinpfalz  la  mjini  Ludwigshafen akizungumzia  kuhusu serikali  ya  siasa  kali  za  mrengo  wa  kulia nchini  Poland  anaadika:

"Inaelekea  kule Poland  wamesahau , kwamba  Umoja  wa  Ulaya  sio tu  kwamba  una  maadili  yake, lakini  pia ni  jamii  inayofuata  haki. Na inaeleweka  pale  Umoja  wa  Ulaya  unakemea mwanachama pale  msingi  wa  utawala  bora  unapokandamizwa kwa  kuondoa uhuru  wa  mahakama. Umoja  wa  Ulaya  haupaswi  tena  kuunga mkono  hali  hiyo,  na  kufanya  kila  linalowezekana  kurejesha  hali katika  njia  yake, ili  kutekeleza  makubaliano  yaliyokwisha  fikiwa."

Akizungumzia  suala  la  SPD kujiingiza  katika  mzozo  wa  wakimbizi unaoutikisa  muungano  wa  vyama  vilivyoko serikalini  vya  CDU na  CSU, mhariri  wa  gazeti  la  Mitteldeutsche Zeitung  anaandika:

"Hakuna mwananchi  ambaye  anaweza  kuelewa , wakati  chama cha  SPD kutokana  na baadhi  ya  vituo  vya  kuwahifadhi  kwa muda  wahamiaji  itavunja  muungano  unaounda  serikali  ya Ujerumani. Pia  kutokana  na  matukio  machache  yanayowahusu wakimbizi SPD kinataka  kuelekeza  hali  hiyo  katika  masuala  ya kiutu  zaidi, na  kusababisha  hatari, kutokana  na  mbinyo  huo.

Chama  cha  SPD kinapaswa kujiweka  mbali  na masuala  fulani, ambayo  waliyaacha  mwaka 2015."

Gazeti  la  Allgemeine Zeitung  la  mjini  Mainz likiandika  kuhusu mada  hiyo  kuhusu  chama  cha  SPD linaandika:

"Chama  cha  SPD kimekuwa kama  mtoto  mdogo, ambapo wamekuwa wakichezea  mchanga pamoja  na  dada zake, ambao wanapigana na  kisha dada hao  wakaanza  kujenga  karsi  la mchanga, sasa nae  anaingilia  kati  kupinga ubora  wa  kasri  hilo."

Mada yetu  ya  mwisho ni  kuhusu uokozi  wa  vijana  waliokwama katika  pango nchini  Thailand. Mhariri  wa  gazeti  la Hessische Allgemeine  la  mjini  Kassel  anaandika  kuhusu kisa  hicho:

"Dunia  inashusha  pumzi  baada  ya  kugundulika  vijana  12  pamoja na  kocha  wao katika  pango  ambamo  walipotea , lakini  bado vijana  hao  hawajatoka  katika  hatari  dhidi  ya  maisha  yao. Bado hali  ni  ya  kutisha, kwa  kuwa  vijana  hao wanapaswa  sasa kufanya  mazowezi  wa  kupiga  mbizi, ili  kuweza  kuokolewa. Inaweza  kuchukua  miezi  kadhaa, hadi  pale  watakapoweza  kuona mwanga  wa  nje."

Ni maoni  ya  wahariri  wa  magazeti  ya  Ujerumani , kama mlivyokusanyiwa   na  Sekione Kitojo.

Mwandishi : Sekione  Kitojo / inlandspresse

Mhariri: Iddi Ssessanga