1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Makadinali wakutana vatikani

4 Machi 2013

Makardinali wa kanisa Katoliki kutoka sehemu tofauti za dunia,wameanza utaratibu wa kumchagua mrithi wa Papa Benefickt wa XVI aliyejiuzulu mwezi uliopita.

https://p.dw.com/p/17ptr
Makadinali wahudhuria mkutano katika ukumbi wa Synod huko VatikaniPicha: Reuters

Zoezi hilo limeanza leo Vatican saa 3.00 asubuhi kwa saa za Vatican sawa na saa 6 mchana kwa saa za Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa New Synod Hall.

Mkutano huo ndio utafungua mchakato wa uchaguzi wa Papa mpya na unatarajiwa kuandaa ratiba ya uteuzi wa papa mpya.Makardinali hao ndio watapanga siku ya kufanyika mkusanyiko wao unaoitwa `Papal Conclave' kwa ajili kufanya uchaguzi huo.

Kutokana na utaratibu wa kanisa Katoloki, uchaguzi wa Papa hutakiwa kufanyika siku 15 hadi 20 kufuatia siku kiti cha papa kilipoanza kuwa kitupu na Uchaguzi kwa kawaida hufanyika katika Kanisa la Sistine Chapel.

Takribani makardinali 115 kutoka nchi mbalimbali duniani,wanahusika na uchaguzi huo wa Papa ambapo Kati ya hao, makardinali 67 waliteuliwa na Papa Benedict,Joseph Aloisius Ratzinger.

Kwa upande wake aliyekuwa papa ambaye ni mzaliwa wa Ujerumani amekuwa akitumia muda kufanya ibada, kusoma vitabu na meseji za kumtakia kila la kheri papa aliejuzulu kutoka sehemu mbalimbali duniani na kutafakari.

Hadi sasa hakuna tarehe yoyote iliotajwa kuhusu uchaguzi huo wa papa ingawa vyanzo vya habari vya Italan vimedokeza kuwa huenda Machi 11 2013 ikawa siku hiyo ya uchaguzi wa papa.

Kiongoazi wa chuo cha makardinali Angelo Sodano ameongea kuwa siku maalumu ya kuanza kwa uchaguzi huo,haitatajwa hadi hapo makardinali wateule wote watakapo wasili mjini Rome

Papa mpya atatokea bara gani?

Vatikan Kardinäle Papst Nachfolge
Kadinali Ricardo Jamin Vidal wa Philippines(kulia) na Luis Antonio Tagle wamewasili kuhudhuria mkutano wa makadinali kabla ya kongamano litakalomchagua Papa mpyaPicha: Reuters

Nafasi ya Papa ajae imeendelea kuwa wazi kwa kila mtu kutoka katika maeneo mbalimbali ya dunia, na kutoka katika makanisa mbalimbali.

"Wakati alipofariki John Paul II mwaka 2005, kila mtu alikuwa anafikiria atakaeshinda nafasi hiyo kwa mwezi huo naku ra ilikuwa muda mfupi tuu'' amesema kadinali alijiuzulu akiongea na shirika la ahabari la AFP.

Kwa upande wa Afrika Makardinali waliotajwa ni pamojana Peter Turkson kutoka Ghana, Robert Sarah Guinea na Wilfrid Napier kutoka Afrika Kusini

Mwandishi: Hashim Gulana / AFP,REUTERS

Mhariri:Hamidou Oummilkheir