1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MALTA:Waafrika 22 wahofiwa kuzama baharini

21 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBpt

Waafrika 22 wanahofiwa kuwa wamekufa baada ya chombo chao cha usafiri kuzama katika bahari ya Mediterania kusini mwa Malta. Waafrika wanne walionusurika waliweza kuokolewa kwa mashua ya wavuvi.

Waafrika hao walikuwa njiani katika jaribio la kutaka kuhamia Ulaya ili kujipatia maisha bora .

Waafrika wengine mia moja walikufa maji ama walipotea mwezi uliopita katika bahari, kati ya Libya na Malta.