1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Manchester City yaipiku Liverpool ubingwa wa Premier League

Sekione Kitojo
13 Mei 2019

Manchester City yatwaa  taji la  Premier League  kwa  mara  ya  pili mfululizo, Liverpool  bado yalazimika  kusubiri kwa  uchungu kunyakua  taji  hilo.

https://p.dw.com/p/3IQov
Premier League: Brighton & Hove Albion v Manchester City
Picha: Getty Images/M. Regan

Manchester City walilazimika  kupambana  hadi  dakika  ya  mwisho baada  ya  kuburuzwa  na  Liverpool  lakini  walipata  njia  na  kurejea ushindi  wao  kama  machampioni nchini  humo. Timu  iliyoshangaza ni Wolves, pia  kuondoka kwa kocha  nyota  Mourinho  na  bila shaka  ni  mshangao  na  masikitiko  makubwa, ni  baadhi  ya matukio  mengine  katika  msimu  huu.

Premier League: Brighton & Hove Albion v Manchester City
Wachezaji wa Manchester City Ilkay Gundogan (kulia) akisherehekea baada ya kufunga baoPicha: Getty Images/M. Regan

Vuta nikuvute  kati ya  Manchester City  na  Liverpool  itatambulika milele kuwa  ni  mpambano  mkali  wa  kuwania  ubingwa  nchini England.

Mvutano  baina  ya  Manchester City  na  Liverpool ambapo  hakuna timu  iliyotaka kupoteza  ulikwenda  hadi  katika  siku  ya  mwisho ya mchezo  wa  msimu  na  pale  vumbi  lilipotulia  ilikuwa  ni  Pep Guardiola  wa  Manchester City  ndie  aliyenyakua taji  hilo kwa mara  ya  pili kwa  mwaka  wa  pili  mfululizo. Na  katika  mkutano  na waandishi  habari Pep Guardiola  alisema.

"Ubingwa mfululizo ni mgumu  sana, kwa  hiyo kwa msimu  wa kwanza  ulikuwa  barabara  kabisa, lakini  msimu  huu  tulikuwa  na mpinzani mgumu  zaidi, kwa  hiyo  nawapongeza  Liverpool pia kwa msimu  mzuri  kabisa, lakini  tumefanikiwa. Tumewashinda."

Premier League: Brighton & Hove Albion v Manchester City
Kocha wa Manchester City Pep GuardiolaPicha: Getty Images/M. Hewitt

Liverpool  ilionekana  kuwa  njiani  kunyakua  taji  hilo  katika  muda wa  miaka  29 wakati  walipokuwa  na  miadi  na  Man City  Januari 3 ikiwa  na  nafasi  ya  kufungua  mwanya  wa  pointi 10. Lakini mabingwa  watetezi  Man City walipambana  na  kupata  ushindi  wa mabao 2-1 na  kurusha  konde  la  kwanza  katika  mpambano  huo wa  vigogo. Ni  kipigo  pekee  cha  Liverpool  katika  msimu  huu na kufungua  mlango  kwa  City , kuchukua  uongozi mwezi  Februari. Kocha  wa  Liverpool  Juergen Klopp  aliipongeza  pia  Man City.

"Inakatisha  tamaa , sio muda wa  furaha, sio  hasa  hivyo, lakini tunao  muda  wa  kutosha  kupata kujua  ni  kitu  gani  na  kuangalia na  kuhisi  pengine kuwa  msimu  huu  ulikuwa  mzuri  sana. Ilikuwa safi  sana,  pointi  97 ni jambo bora sana,  na  ni  kwasababu  tu Manchester City ilikuwapo, basi  haitoshi. Katika  nchi  nyingine ingekuwa  rahisi  na  kutosha, lakini  hapa, hivyo  ndio  ilivyo. Hakuna shida  na  hilo, huo  ni  mpambano ambao  tumo ,  sio  mashindano ya  miaka  ya  30, ya miaka  ya 20 , ama  miaka  10  iliyopita, ni tofauti  kabisa na  vijana  hawa  walikuwa  tayari  kupambana  na nawapa  heshima  zangu. Sio tu  wao  kwasababu  lazima  niseme watu  wengi  wanasema  juu  ya  mashabiki wa  Liverpool , kwamba wanataka  sana  kushinda ligi, na  vitu  kama  hivyo. Vile walivyotufuatilia, inafurahisha. Klabu hii imo  katika  wakati  wake mzuri  sana kwa  muda  mrefu na  haitaishia  hapo  kwasababu  kuna timu  moja  ina  pointi  moja  zaidi."

Jürgen Klopp
Kocha wa Liverpool Juergen Klopp Picha: picture-alliance/PA Wire/P. Byrne

Europa League

Chelsea  ilimaliza ikiwa  nafasi ya  tatu  pointi  25  nyuma  ya Liverpool, lakini ilitosha  kuwapa  nafasi  ya  kucheza  katika Champions League  msimu  ujao pamoja  na  Tottenham.  Arsenal katika  msimu  wao  wa  kwanza  na  kocha  Unai Emery , na Manchester  United  walikuwa  nyuma  wakipata   fursa  ya  kucheza Europa  League.

Lakini  iwapo  Arsenal  itashinda   mchezo  wake  wa  fainali  dhidi ya  Chelsea  katika  Europa  league  itajiunga  na  timu  nne  za England  katika  Champions League  msimu  ujao.

Wolverhamton Wanderres  ilimshangaza  kila  mmoja  kwa  kumaliza nafasi  ya  saba  baada  ya  kurejea  katika  Premier League  na  pia itafuzu  kucheza  katika  Europa  League iwapo  City itashinda kombe  la  FA  Jumamosi katika  fainali  dhidi  ya  Watford, ambayo itapata   nafasi  hiyo  iwapo  itashinda.

Manchester United-Trainer Ole Gunnar Solskjaer
Kocha wa Manchester United Ole Gunnar SolskjaerPicha: Getty Images/C. Ivill

Kocha  wa  Manchester City Pep Guardiola  amezionya  timu nyingine  katika  Premier League  kwamba  mabingwa  hao wataendelea  kuwa  bora  na  imara  baada  ya  kuiweka  kando Liverpool  na  kuwa  timu  ya  kwanza  katika  muda  wa  muongo mmoja  kunyakua mfululizo taji  la  Premier League.

"Hii  ni  ligi  ngumu  kabisa niliyoweza  kushinda kuanzia  mwanzo. Nilishinda  Uhispania, nilishinda  Ujerumani, lakini  hii  ni  ligi  ngumu sana, hususana  ushindani  tuliokabiliana  nao msimu  mzima."

Fussball Champions League Halbfinale l FC Liverpool vs FC Barcelona | Trainer Jürgen Klopp
Kocha Juergen Klopp wa LiverpoolPicha: Getty Images/C. Brunskill

Wakati  hupo  huo  kocha  wa  Liverpool  Juergen Klopp  amewataak wachezaji  wake  kutumia  maumivu  ya  kushindwa  kwao  katika Premier League  kuwa  ni  chachu  ya  kumaliza  msumu  huu  na ubingwa  wa  Champions  League wiki  mbili  zijazo.

Nae  kocha  wa  Manchester  United  moja  kati  ya  timu  vigogo nchini  England  na  barani  Ulaya  Ole Gunnar Solskjaer  amesema timu  yake  itachukua  muda  kuweza  kuziba  mwanya  uliopo  kati yake  na  timu  za  Manchester City  na  Liverpool  baada  ya kumaliza  msimu  huu  kwa  kipigo  cha  mabao 2-0 nyumbani  na Cardiff  City  ambayo  tayari  imeshuka  daraja. United  imemaliza ikiwa  katika  nafasi ya  sita , ikiwa   pointi 32 nyuma  ya  mabingwa Manchester City.

UK Mohamed Salah
Mshambuliaji wa Liverpool Mohamed SalahPicha: imago/Action Plus/D. Blunsden

Wachezaji  watatu  wamefungana  katika  kinyang'anyiro  cha kuwania  kuwa  mfungaji  bora  wa  msimu, ambapo  wachezaji watatu  kutoka  bara  la  Afrika  wamenyakua  kiatu cha  dhahabu katika  kinyang'anyiro  hicho. Wachezaji  hao  ni Sadio Mane, Pierre-Emerick Aubameyang  na  Mohammed Salah.