1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani inahitaji mashujaa kama Martin Luther King Jr.

4 Aprili 2018

Ujerumani ina mashujaa wachache sana nje ya ulingo wa michezo. Inahitaji mashujaa kama King ambao huwapa watu nguvu na ujasiri. Wanasaidia makundi ya vuguvugu kukua ambayo yana nguvu zaidi kuliko watu binafsi.

https://p.dw.com/p/2vSdd
USA Martin Luther King, Jr. National Memorial in Washington
Picha: picture-alliance/newscom/L. Vogel

Huu ni wakati mwafaka wa kutafakari kuhusu dhana ya kukataa tamaduni zinazopendwa, taasisi ama misingi iliyowekwa, anaandika mhariri mkuu wa shirika la utangazaji  Deutche Welle, Ines Pohl.

"Sina furaha katika nchi inayohitaji mashujaa," mwandishi wa Ujerumani wa tamthilia, Bertolt Brecht anaandika kwenye mchezo wake "Maisha ya Galileo," mwisho wa Vita Vikuu vya Pili. Kwa nukuu hiyo, Brecht, mwenyewe alilengwa na Wanazi, alikataa na kupinga tabia ya kuabudu mashujaa katika jamii iliyotawaliwa  kiimla.

Aliamini kwa moyo wake wote kuwa jamii zinazoendeshwa na mfumo wa demokrasia hazihitaji mashujaa kuyatafutia ufumbuzi  matatizo yao. Kinyume chake, wajibu wa watu binafsi hushabikiwa na kukwezwa, na matokeo ya tabia ya kuabudu mashujaa ni utiifu wa kijinga ambao huchangia mmoja kuwa mnyonge.

King anakumbukwa 

Bg 50. Todestag von Dr. Martin Luther King Jr.
Mkewe King Coretta Scott na familia wakimuomboleza, 1968Picha: Flip Schulke. Photo courtesy of UT Austin's Briscoe Center for American History

Martin Luther King Jr. aliuawa miaka 50 iliyopita siku ya Jumatano. Mhubiri huyo hakukata matumani kwenye vita dhidi ya ukosefu wa haki, vita vya Vietnam na kudhulumiwa kwa Waamerika weusi. Yeye na wafuasi wake walijitolea bila ya kutumia nguvu wala ghasia, licha ya kukabiliwa na machafuko  dhidi yao. Hata leo, angali anawatia ujasiri watu ambao wanahisi kutoridhika na uongozi uliopo na wanaoamini kuwa  maisha tofauti yanawezekana.

Hivi karibuni  mji wa Washington, DC, Marekani, maelfu ya watu waliandamana wakipinga ushawishi wa makundi yanayojihusisha na matumizi ya bunduki kwa siasa za Marekani.  Maandamano makuu, yalipangwa na kuongozwa na wanafunzi wa shule ya Parkland, Florida, baada ya wanafunzi wenzao 14 na wafanyikazi watatu wa shule ya upili ya Stoneman Douglas, kuuawa mwezi Februari. Kwenye mhadhara wa kitaifa ulioandaliwa katika mji mkuu, Yolanda Renee King, mwenye umri wa miaka tisa, aliongeza uzito hotuba ya babu yake, "Nina Ndoto" na urithi wa vuguvugu la makundi ya kupigania haki za binadamu ni bayana katika maneno na vitendo vya Emma Gonzalez, mwenye umri wa miaka 18, mmoja wa waandalizi wa mkusanyiko uliopewa jina, " Msafara kwa ajili ya  maisha yetu."

Sio suala la utiifu kuwa na mashujaa kama vile King na watu kama yeye. Watu kama hao wanatupa nguvu na ujasiri. Wanasaidia makundi ya vuguvugu kukua na makundi hayo yana nguvu zaidi kuliko watu binafsi.

Chimbuko la matumaini

Ines Pohl Kommentarbild App
Ines Pohl Mhariri mkuu wa Deutche Welle Picha: DW/P. Böll

Mashujaa kama vile King wanatupa matumaini. Wanatuonyesha kuwa kuna thamani ya kusimama na kuyaacha mazingira tunayopenda, kubainisha ujasiri na kuonyesha umoja; kujenga mitandao na kutovunjika mioyo; na kutikisa watu kutoka kwenye nafasi na hadhi zao kuu na kuwaita kushiriki.

Ni nguvu hizi ambazo Ujerumani na mataifa mengine yanahitaji kuukabili ulimwengu ambao hueleweki na kutovunjika moyo ndani ya mizozo ambayo yaelekea haina ufumbuzi. Hatimaye, ni muhimu kudumisha imani na uwezekano wa taifa linaloendeshwa kwa misingi ya demokrasia ambalo linaruhusu uhuru wa wananchi.  Ulimwengu unamkumbuka Martin Luther King leo — sio tu kwasababu ya yale aliyoyafanikisha wakati wa uhai wake , lakini pia kwasababu ya jinsi anavyozidi kuhitajika.

Mwandishi: Ines Pohl, Shisia Wasilwa

Mhariri: Abdul-Rahman