1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MATUMAINI DAFUR

24 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCFy

KHARTOUM:

Mjumbe maalumu wa UM kwa Dafur, amesema ana matumaini mazuri kwamba vikundi vinavyogombana huko Dafur vyaweza vikafikia mapatano ya kuacha mapigano .Amesema vikundi vilivyokataa hapo kabla mazungumzo, sasa vitayari kujadiliana-hii ni kwa muujibu wa Radio ya Sudan ilivyoripoti hii leo.

Jan Eliasson, mjumbe maalumu wa katibu Mkuu wa UM Ki-moon aliwasili mjini Khartoum, jana usiku.Anatazamiwa kuungana na mjumbe mwenzake wa Umoja wsa Afrika Dr.salim Ahmed Salim kujaribu kufufua utaratibu wa amani huko Dafur.