1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Michuano ya "SportPesa Super Cup" yaanza Dar

Sekione Kitojo
5 Juni 2017

Mashindano  mapya  ya  soka kwa  ajili  ya  timu  za  Afrika  mashariki  yanaanza  leo mjini  Dar Es Salaam  zikihusika  klabu  za  juu  kutoka  Kenya , Tanzania  na Zanzibar.

https://p.dw.com/p/2e9Ia
CECAFA Fussball-Cup
Timu ya Uganda ya URA ikipambana na al-Hilal ya SudanPicha: EBRAHIM HAMID/AFP/Getty Images

Mashindano  hayo  ya  mwanzo  ya  SportPesa Super Cup yanaungwa  mkono  na  mashirika  ya  kandanda  ya  Kenya na Tanzania baada  ya  mashindano  ya  kanda  hiyo yanayotayarishwa  na  shirikisho la  kandanda  la  Afrika  mashariki na  kati, CECAFA  kushindwa  kufanyika  mwaka  jana.  

Mashindano  hayo  yanaanza  rasmi  leo(05.06.2017) ambapo miamba ya  Kenya AFC Leopards  watafungua  mashindano  hayo  kwa  kuumana  na Singida United  ya  Tanzani  bara  katika  uwanja  wa  Uhuru mjini Dar es Salaam. mabingwa  wa  ligi  Tanzania  Dar Young Africans wanapimana  nguvu  na  Tusker  ya  Kenya  katika  mchezo  wa  pili leo  jioni. Timu  nyingine  zinazoshiriki  ni Simba  ya  Tanzania, Jang'ombe  ya  Zanzibar , Gor mahia  na  Nakuru All Stars zote kutoka  Kenya.

Tansania CAF Champions League
Mashabiki wa soka mjini Dar es Salaam wakiingia uwanjani kushuhudia pambanoPicha: DW/G. Njogopa

SuperSport United  ya  Afrika  kusini  imeweza  kutoka  sare  ya mabo 2-2  dhidi  ya  mabingwa  wa  kombe  la  Shirikisho , CAF Confederation Cup  TP Mazembe  ya  jamhuri  ya  Kidemokrasi  ya Congo  jana  Jumapili. Ben Malango   na  Mzambia Rainford  Kalaba walipachika  mabao  na  kuwapa  Mazembe  uongozi  wa  mabao 2 , dakika  26 katika  mchezo  huo  katika  mchezo  wa  kundi D katika mji  wa  kusini  nchini  Congo wa  Lubumbashi. Lakini Aubrey Modiba alirejesha  bao  la  kwnza  na  Teboho Mokoena  alisawzisha  katika dakika  ya 66 akiwanyamazisha  mashabiki  wa  nyumbani.

Thomas Ulimwengu
Mchezaji wa timu ya TP Mazembe Thomas Ulimwengu (Kushoto)Picha: Getty Images/A. Tomura

Nayo St George  ya  Ethiopia  iko ukingoni  mwa  kuingia  katika awamu ya  robo  finali  baada ya  kuishinda  V Club  ya  jamhuri  ya kidemokrasi  ya  Congo  kwa  bao  1-0. Goli  la  Saladin Said lilitosha  kuwazamisha   Vita Club , goli  ambalo  ni  la  sita  kwa mshambuliaji  huyo  hatari , na  akiwa  sasa  anaongoza  idadi  ya wafungaji  mabo  katika  kinyang'anyiro  hicho  barani  Afrika akifuatiwa  na  Msudan Bakary al Madina  wa  El Merrikh   na  Muaid Allafi  wa  Libya   kutoka  Al Ahly Tripoli wakiwa  na  mabao 5.

 

Mwandishi: Sekione  Kitojo / dpae / afpe / ape / rtre

Mhariri: Iddi Ssessanga