1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkuu wa majeshi ya waasi wa Libya ameuawa

Martin,Prema/ZPR29 Julai 2011

Mkuu wa majeshi ya waasi wa Libya, Jenerali Abdel Fattah Younes, ameuawa na kundi la watu waliojihami kwa silaha.

https://p.dw.com/p/RcvS
ARCHIV - Archivfoto vom 16.03.2010 zeigt den von Libyens Machthaber Muammar al-Gaddafi für tot erklärte Innenminister Abdulfattah Junis bei einem Treffen arabischer Innenminister in Tunis (Archiivfoto). Junis, der sich den Aufständischen angeschlossen hat. sagte am Mittwoch (23.02.2011) in einem Telefoninterview des Nachrichtensenders Al-Arabija, ein Anhänger von Gaddafi habe versucht, ihn zu erschießen. Der Schütze habe ihn jedoch verfehlt und stattdessen einen Verwandten des Ministers verletzt. Er sei nun kein Minister mehr, sondern ein Soldat im Dienste des Volkes, fügte Junis hinzu. EPA/STR (zu dpa 0185) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Jenerali Abdel Fattah YounesPicha: picture alliance/dpa

Mwenyekiti wa Baraza la Kitaifa la Mpito la waasi, Mustafa Abdel Jalil amesema, Jenerali Younes alikuwa akirejea Benghazi kutoka uwanja wa mapigano. Viongozi wengine wawili wa waasi pia waliuawa katika shambulio hilo.

Jalil ametangaza siku tatu za maombolezo na amemtuhumu kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi kutaka kuvunja umoja wa waasi. Younes alikuwa waziri wa mambo ya ndani katika serikali ya Gaddafi, lakini alijiunga na waasi katika mwezi wa Februari. Hapo awali, msemaji wa waasi alisema kuwa Younes aliitwa kwenda Benghazi kuhojiwa. Ilishukiwa kwamba Younes aliwasiliana na serikali ya Gaddafi kupitia familia yake.