1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Moscow. Mwandishi wa habari maarufu akutwa ameuwawa.

8 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD51

Mwandishi wa habari za kiuchunguzi ambaye anafahamika kwa taarifa zake za ukosoaji wa serikali ya Russia katika vita na jimbo linalotaka kujitenga la Chechnya amekutwa amepigwa risasi na kufa mjini Moscow.

Polisi wanasema mwili wa Anna Politkovskaya uligunduliwa katika ngazi za jengo anamoishi, pamoja na silaha iliyomuua na risasi nne zilizokwisha tumika.

Amefariki kutokana na kupigwa risasi kadha kwa masafa ya karibu.

Baraza la ulaya limetaka kufanyike haraka uchunguzi kamili wa mauaji hayo.