1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ndege zisizo na rubani kupelekwa DRC

10 Oktoba 2013

Ndege zisizokuwa na rubani maarufu Drones,zitapelekwa mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo mwezi ujao.

https://p.dw.com/p/19xLS
Ndege zisizo na rubani zijulikanazo kama Drones.
Ndege zisizo na rubani zijulikanazo kama Drones.Picha: picture-alliance/dpa

Kamanda wa kijeshi wa tume ya kulinda amani ya umoja wa mataifa nchini Kongo,Monusco amesema kwamba ndege hizo zitahusika na kuchunguza mpaka wa Kongo na Rwanda. Wakati huohuo shirika la kimarekani la Enough Project limetuhumu waasi wa M23 kuendelea na biashara haramu vya madini. Kwenye ripoti yake ilotolewa hii leo shirika hilo limesema kila mwaka waasi hao na washirika wao kutoka Uganda na Burundi wameuza dhahabu ya zaidi ya dola milioni mia tano.

Sikiliza taarifa kamili kutoka kwa mwandishi wetu Salehe Mwanamilongo kwa bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mwandishi: Salehe Mwanamilongo

Mhariri: Saumu Mwasimba