1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu akaidi shinikizo la kimataifa

Tatu Karema
16 Februari 2024

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, amesema leo kwamba nchi yake haitashinikizwa kukubali kuwepo kwa taifa la Palestina.

https://p.dw.com/p/4cURW
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu.
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu.Picha: Ohad Zwigenberg/AP/dpa/picture alliance

Haya yanajiri baada ya ripoti ya gazeti la Washington Post kusema kwamba Marekani, ambayo ni mshirika mkuu wa nchi hiyo, inaendeleza mipango ya kuundwa wa taifa la Palestina.

Katika taarifa iliyochapishwa baada ya kuzungumza kwa njia ya simu na Rais Joe Biden wa Marekani, Netanyahu amesema kuwa Israel inakataa shinikizo za kimataifa na itaendelea kupinga kutambuliwa kwa upande mmoja kwa taifa la Palestina.

Soma zaidi: Viongozi wa dunia waisihi Israel kuacha operesheni ya Rafah

Hapo jana, Washington Post iliripoti kuwa Marekani inashirikiana na baadhi ya nchi za Kiarabu zikiwemo Misri, Jordan, Umoja wa Falme za Kiarabu, Qatar na Saudi Arabia, ambayo Israel imetafuta kwa muda mrefu kuanzisha nayo uhusiano wa kidiplomasia, kuhusu mpango wa baada ya mapigano kwa kanda hiyo, ambao utajumuisha ratiba ya kuanzishwa kwa taifa la Palestina.