1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nusu-finali Kombe la Ulaya

24 Juni 2008

Leo Ujerumani yaumana na Uturuki.Kesho ni zamu ya Spian na Russia.

https://p.dw.com/p/EQA3

Baada ya mapumziko ya siku 2, kombe la Ulaya la mataifa linarudi uwanjani jumatano hii kwa nusu finali ya kwanza-Ujerumani ikicheza na Uturuki,mjini Basel,Uswisi.

Kesho itakua zamu ya Spian iliovunja mwiko wa miaka 88 wa kutowafunga mabingwa wa dunia-Itali kukata tiketi yao ya finali wakitoana jasho na Urusi.Urusi iliipiga kumbo Holland baada ya kurefushwa mchezo.Ni timu gani 2 zitacheza finali ya kombe hili jumapili ijayo ndilo swali analouliza kila mmoja na si rahisi kulijibu kwa jicho la maajabu mengi yaliotokea tangu kuanza kombe hili la Ulaya:

Tukianza na changamoto ya kesho kati ya spain na Russia, ni wazi waspain wamebidi kusahau mpambano wao wa awali na Urusi walipoikomea mabao 4:1 na wanajua wazi kesho itakua timu tofauti sana ile walioichezesha kindumbwendumbwe.Baada ya kuilaza holland chini ya kocha wao mdfachi Guus Hiddink,amepanga mtego mwengine kesho wa kuweana

►◄