1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Obama, Xi wamaliza mkutano wao

9 Juni 2013

Barack Obama na Xi Jinping wamemaliza mkutano wao wa kwanza kati ya China na Marekani, wakiweka hali ya kuelewana na kukubaliana kuhusu sera, na kupata jawabu kuhusu Korea ya kaskazini, hali ya hewa na mtandaoni.

https://p.dw.com/p/18mKX
U.S. President Barack Obama and Chinese President Xi Jinping walk the grounds at The Annenberg Retreat at Sunnylands in Rancho Mirage, California June 8, 2013 The two-day talks at a desert retreat near Palm Springs, California, was meant to be an opportunity for Obama and Xi to get to know each other, Chinese and U.S. officials have said, and to inject some warmth into often chilly relations while setting the stage for better cooperation.
Rais Obama na rais Xi Jinping walipokutana Rancho Mirage 8.6.2013Picha: Reuters

Marais  hao  walitumia saa  nane  pamoja   katika  muda  wa  siku mbili, katika  makundi  ya yaliyokuwa  na  ukaribu  ya  wafanyakazi, katika  chakula  cha  jioni, pamoja  na  kutembea  katika  bustani nzuri  katika eneo  lililotunzwa  vizuri  katika  jangwa  la  Califonia.

Ilikuwa  mkutano  wa  kwanza  kati  ya  China  na  Marekani  tangu Xi  mwenye  umri  wa  miaka  59 kuchukua  madaraka  kamili  ya nchi  hiyo  Machi  na  Obama mbunifu  wa  kupanga  upya diplomasia  ya  Marekani  kuelekea  bara  la  Asia  ambaye anatazamwa  kwa  jicho  la  shaka  shaka  na  China, kuchukua madaraka  katika  kipindi  cha  pili  cha  utawala  wake.

U.S. President Barack Obama (L) and Chinese President Xi Jinping (2nd R) meet at The Annenberg Retreat at Sunnylands in Rancho Mirage, California June 8, 2013. The two-day talks at a desert retreat near Palm Springs, California, was meant to be an opportunity for Obama and Xi to get to know each other, Chinese and U.S. officials have said, and to inject some warmth into often chilly relations while setting the stage for better cooperation.
Obama na Xi Jinping katika kikao cha pamojaPicha: Reuters

Pande  zote  mbili  zilitaka  kulegeza mazungumzo  hayo kati  ya China  na  Marekani  kuwa  ya  kawaida, na  hali  hiyo  imeonekana kufanikiwa. Katika  wakati  fulani  Obama  na  Xi , wakitafuta msimamo  wa  pamoja  kama  wanasiasa , walitayarisha mitazamo yao  katika  kuelekeza  kule  ambako  wanataka  kuyaelekeza mataifa  yao.

Masuala  nyeti

Wakati Xi  alipoondoka  jana  jumamosi(08.06.2013), maafisa  wa  Marekani wamesema , viongozi  hao  wawili  walizungumza moja  kwa  moja kuhusu maeneo  ya  matatizo, usalama  katika  mtandao, wakashutumu mkwamo  kuhusu  mpango  wa  kinuklia  wa  Korea  ya kaskazini  na  kukubaliana  kuhusu  msukumo  mpya  wa  pamoja kuhusu  mabadiliko  ya  tabia  nchi.

Mshauri  wa  masuala  ya  usalama  wa  Marekani  Tom Donilon amesema  mazungumzo  hayo , yalikuwa kabisa  si  rasmi , ya maana na yaliyozungumzia  mambo  mengi  na yenye  mwelekeo mzuri kwaajili  ya  uhusiano  muhimu  wa  mataifa  hayo  mawili yenye  nguvu  duniani , ambao  mara  nyingi  umekuwa katika  hali ya  mivutano  na  ulihitaji  ukarabati  wa  kila  mara.

President Barack Obama gestures with Chinese President Xi Jinping at the Annenberg Retreat at Sunnylands as they meet for talks Friday, June 7, 2013, in Rancho Mirage, Calif. Seeking a fresh start to a complex relationship, the two leaders are retreating to the sprawling desert estate for two days of talks on high-stakes issues, including cybersecurity and North Korea's nuclear threats. (AP Photo/Evan Vucci)
Obama na Xi Jinping wakitembea katika bustaniPicha: picture-alliance/AP

Kansela  wa  taifa  wa  China Yang Jiechi  amesema  viongozi  hao hawakuona  haya  kuelezea  tofauti  zao, ikiwa  ni  pamoja  na mauzo  ya  silaha  ya  Marekani  kwa  Taiwan  na  madai  ya  China ya  maeneo  katika  bahari  ya  kusini  mwa  China.

Hawakuoneana  haya

Obama  na  Xi  wamekubaliana  kufanyakazi  kwa  pamoja kuwezesha  kuzuwia silaha  za  kinuklia  katika  rasi  ya  Korea, kufuatia  majaribio  ya  kinuklia  na  makombora  pamoja  na  onyo kali  la  vita  vya  silaha  za  atomic  vilivyotolewa  na  korea  ya kaskazini , mshirika  mkubwa  wa  China  ambae huleta  usumbufu mkubwa.

Wamefanikiwa  kupata  kwa  kiasi  kikubwa  msimamo  wa  pamoja katika  suala  hilo, Donilon  amesema , na  amesifu  hatua  za  hivi karibuni  zilizofikiwa  na  China  kumpuuzia  kimya  kimya  kiongozi wa  Korea  ya  kaskazini  ambaye  hana  uzoefu Kim Jong-Un.

Obama  wakati  huo  huo ameweka  wazi  kuwa  wimbi  la mashambulizi  ya  China  dhidi  ya  Marekani  katika  mtandao  katika haki  miliki  ya  biashara  nchini  Marekani   pamoja  na  teknolojia  ya kijeshi, litakuwa  suala  linaloleta  utata  katika  uhusiano  baina  ya mataifa  hayo.

Donilon  amesema  kuwa  Xi , alikiri  kuwa  suala  hilo  ni  muhimu kwa  Marekani, na  aliondoka  Califonia  akiwa  hana  shaka  kuhusu wapi  Obama  anasimamia  katika  suala  hilo.

Viongozi  hao  pia  wametoa mwongozo  kwa  makundi  ya maafisa kutoka  kila  nchi  ambao  wanatarajiwa  kukaa  chini  na  kujadili suala  la  udukuzi  katika  mtandao  wa  internet  mwezi  Julai.

Mwandishi : Sekione  Kitojo  /  afpe

Mhariri : Bruce Amani