1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Platini kuongoza UEFA kwa muhula wa tatu

23 Machi 2015

Michel Platini atachaguliwa kuongoza kwa muhula wa tatu kama rais wa shirikisho la kandanda Ulaya – UEFA na kumweka katika mkondo wa kuongeza tajriba yake na hadhi yake kama nguli wa kandanda

https://p.dw.com/p/1EvfY
EM 2020 UEFA Vergabe
Picha: picture-alliance/dpa/Patrick Seeger

Platini mwenye umri wa miaka 59, ana uhakika wa kuchaguliwa tena katika Mkutano Mkuu wa UEFA unaoendelea mjini Vienna, kwa sababu hakuna yeyote kutoka kwa mashirikisho 54 ya kitaifa aliyejitokeza kumpinga.

Baada ya kuchaguliwa kwa mara ya kwanza kuwa Rais wa UEFA mwaka wa 2007, nyota huyo wa zamani wa Juventus na mshindi mara tatu wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka ya Ballon d'Or alirejeshwa uongozini mwaka wa 2011 na tena anachaguliwa kwa mara ya tatu.

Katika uongozi wake wa miaka minane, Platini meimarisha hadhi ya Ligi ya Mabingwa, mojawapo ya tamasha maarufu zaidi na lenye thamani kubwa katika kandanda ulimwenguni. UEFA inasema dimba la mwaka huu litatazalisha euro bilioni 1.34.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman