1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

POTSDAM: Misaada ifungamanishwe na uongozi mzuri

19 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CC0l

Mawaziri wa fedha wa nchi tajiri zilizoendelea kiviwanda duniani-G8 wanakutana nje ya mji wa Potsdam nchini Ujerumani.Miongoni mwa masuala yanayoshughulikiwa,ni njia za kuzuia madeni makubwa ya nchi za Kiafrika.Suala hilo linazingatiwa wakati ambapo Urusi na China zinatoa mikopo mikubwa kwa nchi za Kiafrika. Ujerumani inasema,misaada ifungamanishwe na uongozi mzuri wa kifedha ili kusaidia maendeleo barani Afrika.