1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Chavez atishia kukatiza usafirishaji wa mafuta kwa Marekani

11 Februari 2008
https://p.dw.com/p/D5f9

Rais wa Venezuela, Hugo Chavez, ametishia kukatisha usafirishaji wa mafuta kwa Marekani baada ya kampuni kubwa ya kimarekani ya Exxon Mobil kushinda kuishawishi mahakama itoe amri ya kuzifungia mali za Venezuela za thamani ya dola bilioni 12.

Kampuni hiyo imewasilisha maombi katika mahakama za Marekani, Uingereza na Uholanzi kupinga hatua ya Venezuela kutaifisha visima vyake vya mafuta.

Rais Hugo Chavez ameishutumu Marekani kwa kushirikiana na kampuni hiyo kubwa ya mafuta duniani katika mashtaka hayo na kudai kwamba serikali ya mjini Washington inafanya vita vya kiuchumi dhidi ya Venezuela