1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Duda: Poland iko tayari kupokea silaha za nyuklia za NATO

23 Aprili 2024

Rais wa Poland Andrzej Duda amesema nchi hiyo iko tayari kupokea na kuhifadhi silaha za nyuklia kutoka kwa Jumuiya ya Kujihami ya NATO.

https://p.dw.com/p/4f4Sl
Rais wa Poland Andrzej Duda
Rais wa Poland Andrzej DudaPicha: Hannes P Albert/dpa/picture alliance

Rais Duda amesema yuko tayari ikiwa washirika hao watachukua uamuzi kama huo kwa lengo la kuimarisha usalama katika eneo la Mashariki la Muungano huo wa kijeshi.

Hata hivyo, Waziri Mkuu wa Poland Donald Tusk amesema anahitaji kupata taarifa zaidi juu ya mazingira yayoliyopelekea rais Duda kutoa kauli ambayo amesema ni kubwa na nzito mno. Tusk amesisitiza kuwa mipango yoyote ni lazima iratibiwe kikamilifu na kuhakikisha ikiwa ni uamuzi wa wote.

Mwaka jana, Urusi ilituma makombora ya kimkakati ya nyuklia huko Belarus huku kukiwa na hali ya mvutano kati yake na NATO kufuatia uvamizi wake nchini Ukraine. Poland, ambayo inapakana na Ukraine upande wa magharibi, inachukuliwa kuwa mshirika muhimu wa Kiev  katika vita hivyo.