1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ROSTOCK: Bush amewasili kuhudhuria mkutano wa G8

6 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBuV

Rais George W Bush wa Marekani amewasili katika mji wa mashariki wa Rostock kuhudhuria mkutano wa kilele wa wakuu wa nchi nane zilizostawi kiviwanda G8.

Mkutano huo unatarajiwa kuanza hii leo katika mji wa pwani wa Heiligendamm.

Bush amewasili hapa nchini Ujerumani akitokea Prague mji mkuu wa Jamuhuri ya Czech alikofanya mazungumzo na rais Vaclav Klaus pamoja na waziri wake mkuu Mirek Topolanek.

Akihutubia kikao cha demokrasia na maswala ya usalama mjini Prague rais Bush alimshutumu rais Vladmir Puttin wa Urusi na kutaja kuwa harakati za marekebisho ya demokrasia nchini humo zimekwama.

Rais Bush na rais Puttin watakuwa na mazungumzo ya pande mbili pembezoni mwa mkutano wa wakuu wa nchi za G8.