1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Scholz ataka ushindani sawa biashara ya magari na China

Amina Mjahid
15 Aprili 2024

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amesema soko la Ulaya linapaswa kuruhusu magari kutoka China huku akisema ushindani ni lazima uwe wa haki.

https://p.dw.com/p/4em05
Kansela Olaf Scholz wa Ujerumani akiwasili nchini China
Kansela Olaf Scholz wa Ujerumani akiwasili nchini China.Picha: Michael Kappeler/dpa/picture alliance

Scholz ambaye yuko ziarani  nchini China amesema magari ya China yatapewa nafasi katika soko la Ujerumani lakini akaonya kuhusu utumiaji wa mbinu zisizo za haki za kibiashara.

Ujerumani inafaidika na bidhaa kutokana na mahitaji ya bidhaa kutoka  China kuanzia magari hadi kemikali lakini mahusiano ya nchi hizo mbili yanayumba kufuatia kampuni za Ujerumani kusema zinakumbana na vizingiti visivyo vya haki katika biashara zao nchini China. 

Kansela huyo wa Ujerumani anamalizia ziara yake ya siku tatu nchini China hii leo, aliyoandamana na ujumbe mkubwa wa wafanya biashara na wakurugenzi kadhaa wa kampuni za kijerumani. Katika ziara yake hiyo Scholz pia aliizungumzia Taiwan bila ya kuitaja moja kwa moja akiitahadharisha China kwamba kuionea nchi ndogo ni makosa.