1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

sherehe

Abdu Said Mtullya12 Februari 2011

Wapinzani washerehekea ushindi nchini Misri.

https://p.dw.com/p/10GDo
Wananchi wakiwa katika uwanja wa TahrirPicha: AP

Watu nchini Misri  walisherehekea  usiku kucha baada ya Rais Hosni Mubarak kujiuzulu.

 Watu waliimbia, honi za magari  zilipigwa, fataki ziliwashwa na watu  walikusanyika kwenye uwanja wa  ukombozi wa Tahrir mjini Kairo ili  kufunga sala.

Baada ya kuitawala Misri kwa muda wa miaka 30 Rais Hosni Mubarak alijiuzulu hapo jana kufutia shinikizo kubwa la watu wake. 

Maalfu kwa maalfu ya watu wamekuwa wanaandamana kwa wiki kadhaa kumtaka rais huyo aondoke madarakani.

Jeshi  sasa limechukuwa  mamlaka chini ya uongozi wa Mohammed  Hussein Tantawi ambaye mpaka sasa  bado ni waziri wa ulinzi.

Wakati huo huo mashirika ya habari yamearifu kwamba  Katibu  Mkuu  wa Umoja wa nchi za kiarabu  Amr Mussa atajiuzulu  wadhifa  wake  wiki zijazo.  Bwana Mussa ambae hapo awali aliwahi kuwa waziri wa mambo  ya nje  wa Misri  anazingatiwa kuwa mtu mwenye uwezekano  wa  kuushika wadhifa wa  Rais.