1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Siku 100 akiwa rais: Ahadi tano kuu za Trump

29 Aprili 2017

Donald Trump aliahidi kutimiza ahadi zake za kampeni mara tu  atakapokuwa rais wa Marekani lakini inaoneka kama kuanza kutimizwa kwa ahadi hizo kwa haraka kulitumbukiza serikali kwanye kinamasi.

https://p.dw.com/p/2c7fH
USA Donald Kampagne Rede in Louisville
Picha: Reuters/J. Sommers

Donald Trump aliahidi kutimiza ahadi zake za kampeni mara tu  atakapokuwa rais wa Marekani lakini inaoneka kama kuanza kutimizwa kwa ahadi hizo kwa haraka kulitumbukiza serikali kwanye kinamasi.

Donald Trump akiwa kama mgombea alikuwa hana mjuto na alikuwa na majigambo wakati akiahidi ukuta kwenye mpaka wa Mexico utajengwa na utakuwa wa kupendeza,mpango wa afya wa Obama ni balaa utatenguliwa na kuondolewa, wamarekani wanaofanya kazi kwa bidii ambao wameunguliwa na mfumo wa serikali watarudishiwa kazi zao na utu wao.

Trump bafo ana siku 1,300 zilizobakia madarakani kutimiza ahadi zake alizozitowa katika rodha ya kampeni. Lakini hakuna atakayekanusha ametimiza sehemu kubwa ya ahadi hizo katika siku 100 za kwanza.

Hivi ndivyo hali iiliyo kwa sasa:

1)Kumuweka jaji mhafidhina katika mahakama ya juu : Hili bila ya shaka ni ushindi mkubwa kabisa wa Trumph hadi sasa na linatilia mkazo sababu ya Warepublikan waliokuwa na mashaka kuamuwa kumeza nyongo yao wenyewe na kumpigia kura.Kiti kilicho wazi katika mahakama hiyo ya juu na uwezakano wa nafasi nyengine zaidi kujazwa iikuwa ni hatari kubwa kumchaguwa Mdemokrat. Kama vile ilivyo kwa majaji wenzake mhafidhina wa jimbo la Colorado Neil Gorsuch amechaguliwa kushika wadhifa huo maisha.

Maisha katika mpaka wa Mexico

Grenzanlagen USA Mexiko
Mpaka unaoitenganisha Marekani na Mexico.Picha: Reuters/M. Blake

Kuutenguwa mpango wa afya wa Obama na kuuweka mwengine: Huku ni kushindwa kabisa katika siku zake 100 za kwanza madarakani.Sheria ya huduma za afya ya Obama daima ilikuwa na utata-ilianza kuongezeka umashuhuri wake mara tu baada ya Trump kushinda uchaguzi hapo mwezi wa Novemba mwaka jana na kuja kuwa tatizo kwa Warepuplikan ambao sera yao kuu tokea kupitishwa kwa Sheria hiyo ya kumudu huduma za afya yaani mpango wa afya wa Obama ni kujaribu kuutenguwa.Lakini licha ya kuusakama mpango huo kwa miaka saba ule wakati wa kufanikiwa kwao ulipowadia sheria ya Huduma za Afya ya Marekani (GOP) ambayo ilikusudiwa kuwa mshindani wa mpango wa Obama ulikuja kuanguka kwa ghafla na kuondolewa hata kabla ya kupigiwa kura.

3.Kujenga Ukuta:Trump aliahidi kupambana vikali katika suala la wahamiaji,iwe kisheria au venginevyo.Mbali na wito wake wa kuajiri mawakala wapya 10,000 wa uhamiaji chini ya usimamizi wake mamlaka ya Utekelezaji wa masuala ya Uhamiaji na Forodha(ICE) imeongeza misako yao na kuamua kuwarudisha makwao wahamiaji walioko nchini humo kinyume na sheria hatua ambayo imejumuisha kuzitenganisha familia na kuwarudisha makwao watoto ambao walikuwa na bado kisheria wanahifadhiwa chini ya sera za utawala uliopita.

Na kwa suala la ukuta wenyewe ? Mkuu wa bajeti wa Trump amesema kwamba kupata fedha kwa ajili ujenzi wa ukuta huo katika bajeti ya mwakani kwa serikali jambo hilo ni la "lazima."

Kituo cha matangazo cha "Fox News" kimetangaza ujenzi wa ukuta huo yumkini ukaanza mapema katika kipindi cha kiangazi mwaka 2017.  Lakini suala la kugharimia ujenzi wa ukuta huo linaendelea kuwazozaniwa kati ya rais na bunge la Marekani.

Marekani kwanza

USA Washington - President Donald Trump bei griechischer Unabhänigkeitsfeier
Rais Donald Trump wa Marekani.Picha: Reuters/C. Barria

4.Kuwapiga marufuku Waislamu kuingia Marekani: Sinema ya siku 100 ya kwanza madarakani kwa Trump ilianza hasa wakati aliposaini amri ya rais yenye kuamuru kupiga marufuku kuingia nchini humo kwa raia wowote wale kutoka nchi saba zenye idadi ya kubwa ya Wislamu wawe na viza  au hata kadi za kijani za ukaazi wa Marekani.Maandamano yalizuka katika viwanja vya ndege vyote vikuu nchini Marekani na kesi za madai zikafunguliwa.Warepaplikan waliungana na hata baadhi ya Wademokrat walishutumu amri hiyo ya rais.Wakati mahakama huko San Francisco ilipogunduwa kwamba amri hiyo imekiuka katiba,Trump alidokeza kwamba ataipeleka Mahakama ya Juu.Baadae aliamua kusaini amri mpya ya rais,safari hii akipiga marufuku kuingia nchini kutoka tu nchi sita.Amri hiyo pia imesitishwa na hivi sasa iko mahakamani.

5.Marekani kwanza : Ahadi hii inaweza kutafsiriwa kwa mapana kwa njia mbali mbali -kuyaweka mbele kwanza maslahi ya kiuchumi ya Marekani au kuikwamuwa Marekani katika ahadi zake za sera ya kigeni.Watu wengi walifikiri kwamba ilikuwa imekusudia ahadi ya kulenga kwenye matatizo yalioko ndani ya nchi na kuipuza dunia.

Mmojawapo wa mfano mkubwa kabisa wa ahadi hiyo ni uamuzi wa Trump wa kujitowa katika makubaliano ya ushirikiano kati ya Ulaya,Pasiifiki na Marekani (TTP) ambayo ni makubaliano ya biashara ya kimataifa yenye utata yalioshinikizwa na Obama na Clinton na yaliyojadiliwa kwa miaka mingi na na mataifa 12 ya Asia. Ameyataja kuwa ni "makubaliano mabaya" ambayo yatazidhuru kampuni na wafanyakazi wa Marekani

Hata hivyo inaonekana Trump amejifunza kwamba kuwa kiongozi wa dunia ilio huru inamaanisha uwasiliane nayo kwa kawaida,.Siku 100 za Trump madarakani pia zimeshuhudia shambulio la kijeshi la kwanza la Marekani dhidi ya Syria,kuongezeka kwa mvutano na Korea Kaskazini na kutaka kurudi katika ahadi yake ya kuyatupilia mbali makubaliano ya nyuklia ya Iran aliyoyaita "mabaya".

Uchunguzi wa maoni unadokeza kwamba kambi ya" Marekani kwanza"  bado inamuunga mkono lakini hakuweza kupata wafuasi wapya

Mwandishi :Maya Shwayder/Mohamed Dahman

Mhariri :Yusra Bewayhid