1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

THE HAGUE:Kesi ya Taylor kusikilizwa tena

20 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBXb

Mahakimu wanaohukumu kesi inayomkabili rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor leo wanatarajiwa kutoa uamuzi juu ya lini kesi hiyo itaanza kusikilizwa tena baada ya watetezi wa mshtakiwa kuomba muda zaidi wa matayarisho. Watetezi hao wapya wa bwana Taylor wameomba kesi iahirishwe hadi tarehe 7 januari mwaka ujao.Taylor anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita.

Anadaiwa kuhusika katika vita vya nchini Sierra Leone ambapo watu wapatao laki moja na alfu 20 waliuawa .