1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uasi wa Wagner hautarejesha nyuma upatanishi wa Afrika

27 Juni 2023

Afrika Kusini mesema jaribio la uasi uliofanywa na wapiganaji wa kundi la Wagner nchini Urusi mwishoni mwa juma lililopita halitaathiri juhudi za Afrika za kujaribu kutatua mzozo kati ya Urusi na Ukraine.

https://p.dw.com/p/4T8HH
Annalena Baerbock mit Cyril Ramaphosa Südafrika
Picha: South African Presidency

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Afrika Kusini Naledi Pandor amewaambia waandishi habari kwamba ujumbe wa amani wa Afrika nchini Ukraine na Urusi utasonga mbele licha ya uasi wa Wagner.

Pandor aliyekuwa akizungumza mjini Pretoria akiwa na mgeni wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Annalena Baerbock, alisema ujumbe wa viongozi wa Kiafrika ulikuwa ni ziara ya awali nchini Urusi na Ukraine na kwamba viongozi wa mataifa hayo mawili walikubali kufanya mikutano zaidi katika wiki chache zijazo. 

Soma zaidi: Baerbock kuzungumza na Pandor kuhusu Ukraine

Rais Cyril Ramaphosa na viongozi wengine wa Afrika walizitembelea Kyiv na Moscow mwezi huu kujaribu kutafuta suluhu ya mzozo unaoendelea.

Kwa upande wake, Baerbock, ambaye yuko ziarani nchini Afrika Kusini, amesema uasi uliozimwa nchini Urusi umeonesha Rais Vladimir Putin anaiharibu mwenyewe nchi yake.