1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa yaitandika Brazil, Sweden watinga hatua ya mtoano

Sylvia Mwehozi
29 Julai 2023

Michuano ya Kombe la Dunia la Wanawake inayoendelea huko New Zealand na Australia, Ufaransa wamewachapa mabingwa wa Amerika ya Kusini timu ya Brazil kwa mabao 2-1.

https://p.dw.com/p/4UXZG
Timu ya Ufaransa
Kikosi cha wanawake cha UfaransaPicha: JAMES ROSS/AAP/IMAGO

Michuano ya Kombe la Dunia la Wanawake inayoendelea huko New Zealand na Australia, Ufaransa wamewachapa mabingwa wa Amerika ya Kusini timu ya Brazil kwa mabao 2-1.

Nahodha wa Ufaransa Wendy Renard alifunga bao la pili na la ushindi mnamo dakika ya 83 ya mchezo. Matokeo hayo yameiweka Ufaransa katika uongozi wa kundi F ikiwa na pointi 4. Katika Mechi nyingine ya kundi hilo Jamaica wamemaliza dakika 90 na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Panama.Nigeria yaibabua Australia Kombe la DuniaNigeria yaibabua Australia Kombe la Dunia

Katika mchezo wa awali, Sweden walishinda bao 3-0 ndani ya dakika 7 kabla ya muda wa mapumziko wa kipindi cha kwanza dhidi ya Italia. Matokeo ya mwisho yalikuwa mabao 5-0 na kuipeleka moja kwa moja Sweden katika hatua ya mtoano ya Kombe la Wanawake.