1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUganda

Uganda: Polisi yasitisha mikutano ya siasa ya Bobi Wine

14 Septemba 2023

Polisi nchini Uganda imesitisha kampeni ya kitaifa ya uhamasishaji iliyokuwa ikiendeshwa na chama kikuu cha upinzani nchini humo kinachoongozwa na Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, kwa kosa la kumkosoa rais.

https://p.dw.com/p/4WKAZ
Pichani: Bobi wine akishikiliwa na polisi wakati wa maandamano mjini Kampala Machi 15, 2021
Pichani: Bobi wine akishikiliwa na polisi wakati wa maandamano mjini Kampala Machi 15, 2021Picha: Abubaker Lubowa/REUTERS

Tangu mwanzo, fursa ya nadra aliyopewa kiongozi huyo wa upinzani kuendesha mikutano ya hadhara ya kisiasa nchini Uganda iliwashangaza wengi.

Rais wa chama kikuu cha upinzani Robert Kyagulanyi yaani Bobi Wine  alianza mikutano hiyo katika eneo la kusini magharibi mwa Uganda ambayo ni ngome kuu ya rais Yoweri Museveni hasa kutokana na kwamba  yeye ni mzawa wa eneo hilo la Ankole.

Soma pia:Bobi Wine azinduwa maandalizi kuelekea uchaguzi wa 2026

Hata hivyo Bobi Wine nae anayo nasaba katika eneo hilo kutokana na mke wake anatoka jamii hiyo, alivutia umati mkubwa wa watu katika mikutano yake huko na sehemu zingine za nchi bila kutatizwa na polisi.

Hata hivyo mambo yalianza kumwendea vibaya kufuatia matamshi yaliofasiliwa kueneza chuki za kikabila hasa dhidi ya watu wa jamii ya Ankole.

Alikosolewa na watu mbalimbali kwa matamshi hayo na polisi ikatoa taarifa kuwa ingechunguza matamshi hayo na ingemfungulia mashtaka.  

Polisi kusitisha mikutano ya Bobi wine

Hapo jana polisi iliagiza mikutano hiyo kusimamishwa. Msemaji wa polisi Fred Enanga aliwaambia waandishi wa habari kwamba mikutano yote ya uhamasishwa imesitishwa mara moja.

Bobi Wine
obi wine akiwa kwenye mazungumzo na mwandishi wa Dw Mohammed Kheleef mjini BonnPicha: Mohammed Khelef/DW

Hata baada ya kutishiwa kuwa angekamatwa kutokana na matamshi yake, Bobi Wine aliwataka polisi wathubutu kumkamata kwa matamshi hayoakisema afadhali yeye ambaye hutamka tu kuhusu ukabila tofauti na rais  Museveni ambaye huonyesha waziwazi mapendeleo na ubaguzi wa kikabila.  

"Tunaendelea kuhamasisha watu kwa idhini au bila ya idhini ya Museveni." alisema Bobi wine.

Hapo jana Bobi Wine alikamilisha awamu ya kwanza ya mikutano hiyo mjini Arua kaskazini magharibi mwa Uganda.

Soma pia:Kyagulanyi na Besigye kuungana na vyama vingine vitatu

Mikutano hiyo ilienda sambamba na chama chake cha NUP kufungua rasmi ofisi zake sehemu hizo na kuwatambulisha viongozi wa mashinani wa chama hicho kwa wananchi.