1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uhispania yatwaa kombe la Ulaya katika kandanda.

Mtullya, Abdu Said30 Juni 2008

Uhispania yatamba tena baada ya kusubiri miaka 24 !

https://p.dw.com/p/ET8p
Wananchi wa Uhispania wakisherehekea ubingwa wa Ulaya baada ya kuilaza Ujerumani katika fainali ya kandanda.Picha: picture-alliance/dpa

Uhispania  imebeba  kombe   la  ubingwa wa Ulaya  kwa mara  nyingine  baada ya miaka 24.

Timu hiyo iliibwaga Ujerumani  bao  moja kwa  bila  katika  mechi  iliyochezwa kwenye uwanja  wa mji mkuu wa Austria ,Vienna. Goli la Uhispania lilifungwa  na  Fernando  Torres  katika dakika  ya  33. Timu  ya  Uhispania ilionesha kandanda ya hali ya juu sana kiasi kwamba  Ujerumani  ingeliweza kufungwa mabao mengi zaidi.

Kocha  wa  Ujerumani  Joachim Löw amekiri hayo  na  amempongeza kocha mwenzake wa  timu ya Uhispania  kwa kusema kuwa  hana budi  akubali kwamba wachezaji  wa Uhispania walikuwa  hodari  zaidi. Hatahivyo  kocha huyo  amewapongeza  wachezaji  wake kwa  bidii kubwa  waliyofanya  kwenye mashindano  yote ya wiki sita

Wachezaji  wa   Ujerumani  hawakuwa na turufu  wakati wote. Takwimu zimethibitisha kuwa  waliweza  kuenda sambamba  na Uhispania  kwa muda wa dakika kama 15 tu  kwa  wakati mmoja  na baada ya  hapo walidorora kama alivyosema  nahodha  wa  timu ya Ujerumani Michael  Ballack.

Ballack  amesema   timu yake ilikuwa na nia lakini haikuwa  na  uwezo.

Katika  upande  mwingine  waziri mkuu wa Uhispania bwana Zapatero amesema ushindi  wa timu  yake umeashiria mafanikio ya kwanza  chini ya demokrasia  na amewataka wachezaji wa nchi yake  washike  uzi huo huo  hadi kwenye  mashindano ya kuwania kombe la  dunia mnamo  mwaka 2010  nchini Afrika Kusini. Bwana  Zapatero amesema  ni  heshima  kubwa  kwake kwa  uhispania  kupata  mafanikio  hayo chini  ya uongozi wake  wa kidemokrasia .Amesema  mafanikio makubwa zaidi yapo njiani.



►◄