1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiUlaya

Ujerumani kukumbwa na mdororo wa uchumi 2023

Zainab Aziz
9 Oktoba 2023

Utengenezaji wa bidhaa viwandani ulipungua nchini Ujerumani kwa mwezi wa nne mfululizo hadi kufikia mwezi Agosti, kwa mujibu wa data rasmi zilizochapishwa leo Jumatatu.

https://p.dw.com/p/4XI18
Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz
Kansela wa Ujerumani Olaf ScholzPicha: Fabian Sommer/dpa/picture alliance

Hii inaashiria kwamba Ujerumani - nchi yenye uchumi mkubwa zaidi barani Ulaya - itaumaliza mwaka huu ikiwa katika mdororo wa uchumi.

Wakala wa takwimu nchini Ujerumani, Destatis, unasema pato jumla la taifa lilishuka kwa asilimia 0.2 mwezi uliopita baada ya kushuka kwa asilimia 0.6 mnamo mwezi Julai.

Soma pia:Ujerumani kubana matumizi katika bajeti yake mpya

Hali hiyo ya kuvunja moyo inatokana na kushuka kwa asilimia 6.6 kwenye nishati na asilimia 2.4 katika sekta ya ujenzi.

Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF, limetabiri kuwa Ujerumaniitakuwa ndiyo nchi pekee kati ya mataifa yenye uchumi mkubwa barani Ulaya kuingia kwenye mdororo wa uchumi mwaka huu wa 2023.