1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yalaani ongezeko la ghasia dhidi ya UNRWA

10 Mei 2024

Ujerumani imelaani ongezeko la ghasia dhidi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, huko Jerusalem Mashariki.

https://p.dw.com/p/4fiij
Shambulizi kwenye ofisi za UNRWA
Makao makuu ya Shirika la UNRWA yaliyoko Jerusalem Mashariki yamekumbwa na matukio ya kuchomwa moto Picha: Ahmad Gharabli/AFP via Getty Images

Ujerumani imelaani ongezeko la ghasia dhidi yaShirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, huko Jerusalem Mashariki, baada ya shirika hilo kuzifunga ofisi zake kwa muda kufuatia mashambulizi ya mara kwa mara.

Wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani imeandika kupitia ukurasa wa mtandao wa X kwamba Israel inapaswa kuhakikisha ulinzi wa vituo vya Umoja wa Mataifa na wafanyakazi wake katika eneo linalokaliwa la Wapalestina.

Soma pia: Ripoti ya Colonna yasema Israel haijatowa ushahidi kuhusu tuhuma za kuwahusisha wafanyakazi wa UNRWA na shambulio la Oktoba 7

Mkuu wa Shirika la UNRWA, Philippe Lazzarini alitangaza siku ya Alhamisi kwamba wanafunga kwa muda ofisi zao, baada ya Waisraeli kuchoma moto karibu na maeneo ya ofisi za shirika hilo, katika mashambulizi ya hivi karibuni. Mamlaka ya Palestina, Jordan na Saudi Arabia nazo pia zililaani ghasia hizo.