1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Mataifa waongeza muda wa misaada Syria

10 Julai 2021

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeidhinisha kwa pamoja nyongeza ya muda wa kupeleka misaada ya kiutu kutoka Uturuki hadi kaskazini magharibi mwa Syria.

https://p.dw.com/p/3wIej
Syrien Idlib Sorgen vor Schließung des einzigen Grenzübergangs Bab al-Hawa
Picha: Juma Mohammad/IMAGESLIVE/ZUMAPRESS.com/picture alliance

Nyongeza hiyo ya miezi sita itafuatiwa na miezi mingine sita baada ya makubaliano kati ya Marekani na Urusi makubaliano ambayo Umoja wa Mataifa unasema yatatoa fursa ya misaada itakayookoa maisha ya watu milioni 3.4 wanaohitaji misaada ya chakula na kiutu.

Suala la misaada kupelekwa kaskazini magharibi mwa Idlib eneo ambalo limeshikiliwa na waasi, limekuwa kipau mbele cha Rais Biden na alilizungumzia katika mkutano wake wa kilele na Rais Vladimir Putin mwezi uliopita.