1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Walinzi wa mbuga walipwe vyema wanapowakamata majangili

Sekione Kitojo Antonio Arede-Cascais
17 Mei 2019

Shirika la ulinzi wa wanyama duniani WWF linataka walinzi wa wanyama pori katika mbuga za taifa kwenye mataifa ya Afrika walipwe fedha maalum kwa kuwakamata majangili.

https://p.dw.com/p/3IfIL
Black Mamba
Picha: Jeffery-Barbee

Baadhi ya wakosoaji wa utaratibu huu  wanasema hii ni kuhimiza watu kukamatwa bila makosa, utesaji na  mauaji. Kwa  hatua hiyo wakosoaji wanasema  shirika hilo la WWF linataka kuwasaidia walinzi wa mbuga mbalimbali za wanyama barani Afrika, kutekeleza ukatili  dhidi ya raia waishio karibu na mbunga hizo. Na hata wananchi wa mataifa ya Umoja wa Ulaya wanabeba lawama  hizo kwa kuwa kodi zao zinasaidia ukatili huo.

"Tunafuatiliwa  na  kutishiwa, amelalamika  mwanamke  mmoja  wa kabila la  Baka  katika  eneo  la  bonde  la  mto  Kongo. Wanaharakati wa  shirika  la  kutetea  haki  za  binadamu  la  Survival International limekuwa  likikusanya  kwa  muda  wa miaka  mingi kauli  hizo  za mashahidi na  kuandika  ripoti ya  ukosoaji  kuhusiana  na  ukiukaji  wa haki  za  binadamu  wanaofanyiwa  wakaazi  wa  asili  katika  maeneo ya  hifadhi  ama  mbuga  za  taifa  za  wanyama  katika  eneo  la  misitu ya  mvua  katika  Afrika  ya  kati. Katika  miaka iliyopita malalamiko  ya wakaazi  wa  kabila  la  Baka yameongezeka.

Eneo  lao unakutikana msitu wa  Messok Dja katika  Jamhuri  ya  kidemokrasi  ya  Congo , ambao kwa sasa  uko chini  ya  uangalizi  wa  shirika  la ulinzi  wa wanyama  duniani  WWF na  kubadilishwa  kuwa  mbuga  ya  taifa. Eneo  hilo limetengwa  maalum kwa  kuwalinda  sokwe na  kuwa  ni eneo muhimu  kwa kuwalinda  tembo  barani  Afrika. Mradi  huo  unapata fedha  kutoka  kwa  walipa  kodi  wa  Umoja  wa  Ulaya  na  Ujerumani.

Ndovu ni miongoni mwa wanyama wa porini waliko katika hatari ya kuangamia
Ndovu ni miongoni mwa wanyama wa porini waliko katika hatari ya kuangamiaPicha: CC BY 2.0/Benh LIEU SONG

Lakini  wakaazi  wa  eneo  hilo  wanauchukia  mradi  huo: Watu  wa kabila  la  Baka  wanahisi kwamba mbuga  hiyo ya  taifa  inasababisha wao  kubughudhiwa. Licha  ya  kwmba  wameishi  vizazi na  vizazi katika  msitu  huo  wa  Messok Dja.

"Mimi  ni  Mbaka, baba yangu ni Mbaka, mama  yangu  ni Mbaka. Mababu  zetu wametuachia  msitu  huu. Chakula  chetu kinatokana  na msitu huu. Tukiwa  wagonjwa , tunakwenda  msituni  kutafuta dawa katika  msitu huu, na  hata  watoto  wetu  siku zijazo watakwenda kutafuta  chakula  katika  msitu huu. Lakini sasa  tumezuiwa  kuingia katika  msitu huu."

Watu  wa  kabila  la  Baka wameporwa uwezo  wa  maisha  yao. Kwa mujibu  wa  Survival  International wakaazi  wengi  zaidi  wa asili  katika maeneo  ya misituni  barani  Afrika  watakuwa  wahanga wa mradi kama  huu usio na  maadili wa ulinzi wa maeneo  ya  asili. Shirika  hilo limetoa  hadharani  katika  miaka  iliyopita  kila mara  picha  mpya, vidio na ushahidi  wa  maelezo  ya  wakaazi  wenyewe, ambapo limeripoti kuhusu  ukiukwaji  wa  haki  za  binadamu  kupitia  mradi  huo  wa kuwalipa walinzi  wa  mbunga  za  wanyama  katika mataifa ya Jamhuri ya  kidemokrasi  ya  Congo, Cameroon  ama  Jamhuri  ya  Afrika  ya kati. Malalamiko  hayo  kuhusu  kamata kamata holela ni pamoja  pia  na utesaji pamoja  na mauaji  ya  kupangilia.

Maafisa wa wanyama pori nchini Kenya wakitumia helikopta katika shughuli zao kuwahudumia wanyama pori katika mbuga ya kitaifa wanyama ya Nairobi.
Maafisa wa wanyama pori nchini Kenya wakitumia helikopta katika shughuli zao kuwahudumia wanyama pori katika mbuga ya kitaifa wanyama ya Nairobi.Picha: Getty Images/AFP/T. Karumba

Moja  kati  ya  malalamiko  makubwa , ni  kwamba  walinzi  wa  mbuga za  wanyama  wanapata  fedha  kwa  kila  mtu atakayekamatwa. Kutokana  na  malipo  hayo walinzi  wa  mbuga  za  wanyama  wanapat hamasa  zaidi  ya  kukamata watu  wengi  zaidi ambao  hawana  hatia. Linda Poppe  wa  ofisi  ya  Survival International  mjini  Berlin alipozungumza  na  DW alisema.

"Mfumo  huu  wa  kulipa  fedha  kwa walinzi  wa  mbuga za wanyama,unachochea  walinzi  hao  kukamata holela watu  na kuongeza  matumizi  ya  nguvu  katika  eneo  hilo. Fedha  za  kuwalipa walinzi  hao  katika suala  la  msitu wa  Messok-Dja zinatoka  Umoja  wa Ulaya."

Maafisa wa wanyama pori Kenya wakitizama mzoga wa mnyama aliyeuawa na majangili katika mbuga ya Tsavo
Maafisa wa wanyama pori Kenya wakitizama mzoga wa mnyama aliyeuawa na majangili katika mbuga ya TsavoPicha: picture-alliance/dpa

Serikali  ya  Ujerumani  inatoa  fedha  kwa  ajili  ya  eneo  la  bonde  la mto  Kongo  na  kuwezesha  kile  kinachoitwa  malipo  ya  kazi kwa walinzi wa mbuga  ya  wanyama  ya  Salonga , ambao  pia  wanapatiwa fedha  hizo maalum. Immo Fischer , msemaji  wa  WWF  nchini Ujerumani  akijibu  swali  la  DW amesema:

"Fedha za kuwalipa walinzi  wa  mbuga  za  wanyama , ni jambo  la kawaida  na  linatumika  katika  nchi  nyingi  za  Afrika. Walinzi  wa mbuga za wanyama wanafanya  kazi za hatari  sana, na  muhimu sana, na kutokana  na  kazi  hizo  muhimu matokeo  yake  ni  malipo."

Mtu anapaswa  kutambua  kuwa , wazo  hili  limetokana  na  haja  ya kupunguza rushwa. Wakati mlinzi wa  mbunga  ya  wanyama akimkamata jangili na  jangili  huyo ana pembe  mbili  kwa  mfano  za tembo, malipo yake  ya mwaka yataongezeka haraka. Kwa malipo  haya kwa walinzi wa mbuga za  taifa tunataka  kuepuka, kuachiliwa  huru kwa majangili kwa  kuwapa rushwa walinzi.

 

Mhariri: Grace Patricia Kabogo

 LINK: http://www.dw.com/a-48767929