1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanariadha wawili wa Kenya wako taabani

27 Agosti 2015

Wanariadha wawili wa Kenya wamegunduliwa kuwa walitumia dawa za kuongeza nguvu mwilini katika mashindano ya riadha ya IAAF yanayoendelea mjini Beijing, China. Wanariadha hao wamepigwa marufuku ya muda

https://p.dw.com/p/1GMdK
China Leichtathletik WM Joyce Zakary
Picha: Getty Images/A. Lyons

Shirikisho la Kimataifa la Riadha – IAAF limesema kuwa Koki Manunga na Joyce Zakary wamepigwa marufuku kwa muda baada ya kutumia dawa hizo.

Wanariadha hao wa mita 400 walilengwa kabla ya kushiriki katika mbio hizo katika hoteli yao mnamo tarehe 20 na 21 Agosti kulingana na taarifa hiyo ya IAAF

Shirikisho la Riadha Kenya limethibitisha kuwa limefahamishwa kuhusu vipimo hivyo vya IAAF vilivyobaini matumizi ya dawa za kusisimua misuli dhidi ya wanariadha hao wawili. Taarifa ya AK, imesema tayari shirikisho hilo limekutana na IAAF na wanariadha hao wawili na kuanzisha uchunguzi wa hali iliyosababisha matokeo hayo na hatua muafaka itafuata nchini Kenya.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP
Mhariri: Mohamed Khelef