1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wasierre leone wapiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa

5 Julai 2008

-

https://p.dw.com/p/EWxo

FREE TOWN

Shughuli ya kupiga kura katika uchaguzi wa serikali ya mitaa inaendelea nchini Sierre Leone huku kukiwa na ulinzi mkali wa maafisa wa polisi. Uchaguzi huo unaangaliwa kama ni mtihani unaopima umaarufu wa rais Ernest Koroma.Taarifa zinasema ni idadi ndogo ya a watu waliojitokeza kupiga kura kufuatia ghasia zilizokuwa zikishuhudiwa wakati wa kampini.Katika kipindi cha wiki kadhaa zilizopita kumekuwepo taarifa za kuenea ghasia pamoja na vitisho kutoka kwa wafuasi wa chama tawala cha All Peoples Congress APC dhidi ya wapinzani.Sierra Leone mojawapo ya nchi maskini kabisa duniani inajitahidi kujijenga upya baada ya muongo mmoja wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyosababisha kuuwawa watu 120,000 na maelefu ya wengine wakiwa wamekatwa katwa viuongo vya mwili.