1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 10 wauawa DRC kufuatia shambulizi la ADF

Sekione Kitojo
8 Januari 2019

Raia wanane wameuawa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia shambulizi linalodaiwa kufanywa na kundi la ADF.

https://p.dw.com/p/3BBEp
Demorkatische Republik Kongo - Soldaten der Democratic Republic of Congo nach Kämpfen mit Rebellen
Picha: Reuters/G. Tomsaevic

Kiasi  ya  raia  wanane  ikiwa  ni  pamoja  na  jamaa za wanajeshi wameuwawa  katika  mashambulizi  yaliyofanywa usiku  na  watu  wenye  silaha  katika  eneo  tete  la mashariki  mwa  Congo, jeshi  limesema leo.

Watu  wanane  wameuwawa  ikiwa  ni  pamoja  na  wanne ambao  ni  ndugu  wa  wanajeshi, katika  wilaya  ya  Mavivi kaskazini  mwa  eneo  la  Beni, msemaji  wa  jeshi  wa jimbo  hilo  Mark Hazukay  ameliambia  shirika  la  habari  la Ufaransa  AFP.

Polisi  imeweka  idadi  ya  waliouwawa  kuwa  ni  10, baada ya  hapo  kabla  kutangaza  kuwa  waliouwawa  ni  wanane.