1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zambia yanusurika;Ooh La-laah Bukina Faso

26 Januari 2013

Cheche zilionekana jana Ijumaa(25.01.2013)katika mapambano ya mzunguko wa pili katika fainali za kombe la mataifa ya Afrika, AFCON 2013,wakati Burkina Faso ilipoirarua Ethiopia,kwa mabao 4-0.

https://p.dw.com/p/17Rt0
epa03092408 Kennedy Mweene of Zambia celebrates his team first goal during the Africa Cup of Nations match between Zambia and Sudan in Bata, Equatorial Guinea, 04 February 2012. EPA/STR EDITORIAL USE ONLY +++(c) dpa - Bildfunk+++
Mlinda mlango wa Zambia Kennedy MweenePicha: picture-alliance/dpa

Yalitokea pia mabishano makali kuhusu adhabu ya penalti, kadi nyekundu ilitolewa na penalti kuwekwa wavuni na mlinda mlango.

Michezo miwili ya kundi C katika uwanja wa Nelspruit, ikiangaliwa na kundi kubwa kabisa la mashabiki kuweza kuonekana katika wiki ya kwanza ya michuano hiyo, ilifunguliwa na pambano kati ya mabingwa watetezi Zambia dhidi ya Nigeria.

FIFA WORLD CUP 2010 TEAMS Picture taken 14 November 2009 of team Nigeria prior to the FIFA World Cup 2010 qualification match against Kenya in Nairobi, Kenya. Back from left: John Obi Mikel, Obinna Nwaneri, Michael Eneramo, Aiyegbeni Yakubu, Seyi Olofinjana, Joseph Yobo. Front from left: Onyekachi Apam, Peter Odemwingie, Ebenezer Ajilore, Uwa, goalkeeper Vincent Enyeama. Nigeria is among the 32 teams that qualified for the FIFA World Cup 2010. EPA/STAFFORD ONDEGO
Timu ya taifa ya NigeriaPicha: dpa

Emmanuel Emenike wa Nigeria aliandika bao kwa vigogo hao wa soka la Afrika baada ya John Obi Mikel kushindwa kuweka wavuni mkwaju wake wa penalti katika kipindi cha kwanza.

Nigeria's John Obi Mikel during their African Cup of Nations Group C soccer match against Benin at the Ombaka National Stadium in Benguela, Angola, Saturday Jan. 16, 2010. (AP Photo/Themba Hadebe)
Mchezaji wa Nigeria John Obi MikelPicha: AP

Mweene awa shujaa

Lakini gumzo lilizuka pale Zambia ilipozawadiwa penalti ambayo ilionekana kuwa ni ya shaka shaka. Mlinda mlango wa Zambia Kennedy Mweene alikimbia toka langoni mwake na kwenda kuuweka wavuni mpira huo na kuandika bao la kusawazisha kwa timu yake, na kujipatia umaarufu wa kuwa mbabe wa kulinda lango na pia kupachika mabao ya penalti.

Mweene mara nyingi huwa mpigaji wa penalti katika timu yake ya Free State Stars , ya Afrika kusini , na alipachika bao katika mpambano uliomalizika kwa penalti ya ushindi kwa Zambia katika fainali za mwaka jana za kombe la mataifa ya Afrika , dhidi ya Cote D'Ivoire.

Pia ni bingwa wa kuzuwia mikwaju ya penalti, kama alivyothibitisha wakati alipomkatalia Gervihno mwaka jana na tena siku ya Jumatatu pale alipomzuwia Salahadin Said wa Ethiopia kukwamisha mpira wa penalti wavuni.

Nahodha wa Nigeria ambaye pia ndie mlinda mlango wa timu hiyo Vincent Enyeama amekasirishwa mno na uamuzi wa fera kutoka Misri Grisha Ghead. Ni uamuzi mbaya kabisa niliowahi kuona katika historia ya soka, amesema Enyeama.

Baada ya sare hiyo Burkina Faso ilikabiliana na Ethiopia katika uwanja ambao nahodha wa timu ya taifa ya Zambia , Chipolopolo, Christopher Katongo ameuelezea kuwa uwanja mbaya kabisa katika Afrika kusini:

Ethiopia ilianza kwa kishindo, lakini mara tu Burkina Faso ilipoweka mguu vizuri hakuna kilichoweza kuwazuwia wakati Alain Traore alipochangia mabao mawili katika kipigo cha mabo 4-0 dhidi ya Ethiopia.

Ushindi huo ulikuwa mtamu zaidi ukitilia maanani kuwa Burkina Faso ilicheza na watu kumi uwanjani wakati mlinda mlango Abdoulaye Soulama alipoonyeshwa kadi nyekundu.

Ivory Coast's defender Emmanuel Eboue vies with Togo's forward Serge Gakpe during the 2013 African Cup of Nation in Rustenburg on January 22, 2013 at Royal Bafokeng Stadium in a Group D match. AFP PHOTO / ALEXANDER JOE (Photo credit should read ALEXANDER JOE/AFP/Getty Images)
Cote D'Ivoire itapimana nguvu leo na TunisiaPicha: AFP/Getty Images

Leo ni zamu ya Tembo wa Cote D'Ivoire wakitunisha misuli dhidi ya Tunisia na Algeria ina miadi na Togo.

Bundesliga mchezo wa 19

Katika Bundesliga mchezo wa 19 ulianza jana wakati mabingwa watetezi Borussia Dortmund iliiadhibu Nuremberg kwa kuichapa mabao 3-0 nyumbani.

Borussia Dortmund's Jakub Blaszczykowski and Lukasz Piszczek (R) celebrate a goal against Nuremberg during the German Bundesliga first division soccer match in Dortmund January 25, 2013. REUTERS/Ina Fassbender (GERMANY - Tags: SPORT SOCCER) DFL RULES TO LIMIT THE ONLINE USAGE DURING MATCH TIME TO 15 PICTURES PER GAME. IMAGE SEQUENCES TO SIMULATE VIDEO IS NOT ALLOWED AT ANY TIME. FOR FURTHER QUERIES PLEASE CONTACT DFL DIRECTLY AT + 49 69 650050
Wachezaji wa Borussia Dortmund wakipongezana baada ya kupata bao dhidi ya FC NürnbergPicha: Reuters

Michezo hiyo inaendelea leo jioni ambapo Borussia Moenchengladbach inaumana na Fortuna Dusseldorf, Eintracht Frankfurt inaikaribisha Hoffenheim, FC Augsburg ina miadi na Schalke 04, Mainz inasafiri kwenda kukumbana na Sport Verreinnigung Greuther Fuerth na Freiburg ni wenyeji wa Bayer Leverkusen. Hapo kesho, Bayern Munich inayoongoza ligi hiyo inatiana kifuani na Stuttgart, na Hamburg Sport Verein iko nyumbani kuikaribisha Werder Bremen.

Mwandishi ; Sekione Kitojo /afpe