1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zanzibar kutumia shilingi bilioni 7.5 kwa uchaguzi

Salma Said13 Oktoba 2015

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) inasema uchaguzi wa mwaka huu utagharimu jumla ya shilingi bilioni 7.5 hadi kukamilika, huku wadau wa uchaguzi wakiwa na mashaka ya kurejelewa mambo yaliyotia doa chaguzi zilizopita.

https://p.dw.com/p/1Gn8T
Mkurugenzi wa ZEC, Salim Kassim.
Mkurugenzi wa ZEC, Salim Kassim.Picha: DW

ZEC inasema imejipanga kuwaita wadau wa uchaguzi kuwaeleza ukamilishaji wa taratibu za uchaguzi ambazo zinakaribia kufikia ukingoni mnamo tarehe 25 Oktoba, huku masuali kadhaa ya khofu na kasoro za uchaguzi huo yakiibuka kutoka kwa wanasiasa kuhusiana na matayarisho hayo.

Katika kikao cha pamoja cha maandalizi ya uchaguzi kati ya ZEC na wadau wa vyama vya siasa, Mwenyekiti wa Tume hiyo Jecha Salum amesema serikali imetenga jumla ya shilingi billioni 7. 5 kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Zanzibar na tayari tume imeshaingiziwa shilingi billioni 2.5 hadi sasa.

Mwenyekiti huyo alisema katika kuhakikisha wamejipanga vyema wametenga kituo maalumu cha kutangazia matokeo ya uchaguzi, na Makamo wake, Abdulhakeem Ameir Issa, amelitaja eneo hilo kuwa ni hoteli ya Bwawani.

Sikiliza mahojiano kati ya Salma Said na Mkurugenzi wa ZEC, Salim Kassim.