1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Abiy Ahmed aapa kuyavunja majeshi ya mikoa

Mohammed Khelef
10 Aprili 2023

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed ameapa kuvivunja vikosi vya kikanda vilivyoanzishwa na baadhi ya majimbo, akionya kwamba hatua za utekelezaji wa sheria zitachukuliwa dhidi ya upinzani wowote utaokwamisha hatua hiyo.

https://p.dw.com/p/4PrxM
Äthiopien Tigray-Region | zerstörter Panzer
Picha: EDUARDO SOTERAS/AFP/Getty Images

Abiy ameonya kwamba uamuzi huo utatekelezwa hata kwa kulipa gharama kwa ajili ya umoja wa taifa hilo na amani ya watu wake. Mpango huo uliotangazwa kwa mara ya kwanza siku ya Alkhamis unalenga kuleta utangamano katika vikosi hivyo ambavyo vilianzishwa na baadhi ya majimbo.

Soma zaidi: Abiy Ahmed atangaza uwezekano wa mazungumzo na waasi wa Oromo
TPLF yaondolewa katika orodha ya makundi ya kigaidi Ethiopia

Vikosi hivyo vimezua mzozo siku za nyuma, hasa wakati wa vita vya kikatili vya Tigray, huku maafisa wa usalama wanaohudumu katika eneo la Amhara wakishutumiwa kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.

Pande zote za mzozo zimeshutumiwa kutenda uhalifu wa kivita na wachunguzi wa Umoja wa Mataifa.